RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO KUMBUKUMBU YA MASHUJAA WALIOPIGANA VITA VYA KAGERA MKOANI KAGERA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO KUMBUKUMBU YA MASHUJAA WALIOPIGANA VITA VYA KAGERA MKOANI KAGERA

MAS01Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka Mkuki katika Mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa wa Vita vya Kagera uliopo Kikosi cha Jeshi cha Kaboya, Mkoani Kagera leo Julai 25, 2013 MAS1Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Bukoba, Mhashamu Baba Askofu Methodius Kilaini akisoma Sala kwa niaba ya Waumini wa Kanisa Katoliki katika Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa waliopigana Vita vya Kagera Mwaka 1978 hadi 1979. Sherehe hizo zimefanyika leo Julai 25, 2013 katika Kikosi cha Jeshi cha Kaboya, Mkoani Kagera ambapo Mgeni Rasmi ail kuwa ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho KikweteIMG_0286Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishikana Mkono na Askari wa Jeshi la Magereza mwenye Cheo cha Stafu Sajini ambaye alipigana Vita vya Kagera Mwaka 1978 hadi 1979. Sherehe hizo zimefanyika leo katika Kambi ya Jeshi ya Kaboya, Mkoani Kagera MAS2Baadhi ya Mawaziri wa Wizara mbalimbali wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(Mstari wa mbele)waliohudhuria Sherehe za Maadhimisho ya Kumbukumbu za Mashujaa waliopigana Vita vya Kagera mwaka 1978 hadi 1979. Sherehe hizo zimefanyika katika Kambi ya Jeshi ya Kaboya Mkoani Kagera na Mgeni Rasmi alikuwa ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. MAS4Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameongozana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange pamoja na Wakuu Wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama akiwemo Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja alipokuwa akitembelea sehemu walipozikwa Mashujaa wa Vita vya Kagera leo Julai 25, 2013 katika Kikosi cha Jeshi cha Kaboya, Mkoani Kagera MAS5Gadi iliyoundwa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika Gwaride Rasmi la Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa waliopigana Vita vya Kagera mwaka 1978 hadi 1979. Sherehe hizo zimefanyika leo katika Kikosi cha Jeshi cha Kaboya, Mkoani Kagera ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete(Picha na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages