Tigo, American Garden wa-surprise watoto katika ‘Happy Birthday’ ya Andrew Chale - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tigo, American Garden wa-surprise watoto katika ‘Happy Birthday’ ya Andrew Chale

 Andrew Chale akiwa katika Picha ya Pamoja na Watoto ambapo walipewa zawadi mbalimbali na Kampuni ya Simu Za Mikononi ya TIGO
 Hii ndio Keki Iliyokatwa na Mdau Andrew Chale aliyesherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake na watoto waishio kwenye mazingira magumu
 Mdau Andrew Chale akikata keki tayari kwa kugawa kwa watoto waliohudhuria katika hafla fupi hiyo
Mtoto Mashaka Juma wa kituo cha Mitindo House, akimlisha keki kwa niaba ya watoto wenzake zaidi ya 50 waliojitokeza wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwandishi wa gazeti hili Andrew Chale,  jana iliyofanyika ndani ya viunga vya Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na kampuni ya Tigo Tanzania na American Garden.
 Watoto wakishangilia na kufurahia pamoja  na Mdau Andrew Chale
Wenceslaus Kisarika ambae ni Marketing Manager wa K&K pamoja  Cons  Ltd, akifungua shampeni 

KAMPUNI ya Tigo Tanzania leo Oktoba 21, imeweza kufanya ‘surprise’ mbalimbali kwa watoto waliojitokeza katika siku maalum ya kuzaliwa kwa mdau na mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima na blog, Andrew Chale, iliyofanyika ndani ya viunga vya Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam.

Katika party hiyo maalum, Andrew Chale amesema ni ya kwanza kabisa kwa Mtanzania kufanya hivyo kwani ilianza tokea           Oktoba Mosi  kwa kutembelea vituo vya watoto waishio kwenye mazingira magumu na hatarishi  na kutoa misaada na pia kutembelea watoto mahospitalinio na kuwafariji.

Akielezea mtandao huu, Andrew Chale anasema alimwamini Mungu muda wote ndio maana ameweza kufika hapo na pia kutumia nafasi hiyo kwa pamoja kufurahi na watoto hao wakiwemo wale waishio kwenye mazingira magumu.

“Leo, ni siku muhimu sana kwangu, najiona nipo na mamilioni ya marafiki kwa kufika kwenu kumenitia sana faraja Mungu awabariki nyote” alisema Andrew  wakati akiwashukuru watoto mbalimbali waliojitokeza kufanya nao sherehe hiyo.

Watoto hao wakiwemo waliotoka kwenye vituo vya kulelea watoto vikiwemo vya  Tanzania Mitindo House kilicho chini ya Mbunifu,Khadija Mwanamboka, New Life Orphanage center  cha Kigogo, watoto waishio mitahani na wale wa majumbani walijumuika kwa pamoja na kufurahia na ‘Uncle’ wao Andrew Chale  ikiwemo kutembelea sehemu kadhaa za ndani ya jumba hilo la kumbukumbu na kujionea mambo mbalimbali.

Furaha hiyo ya siku maalum ya kuzaliwa kwa Andrew Chale imeweza kuongezwa utamu na kampuni ya Mawasiliano ya mtandao wa simu nchin, Tigo Tanzania, ambayo iliwezesha kumpatia keki na shampeni  maalum pamoja na zawadi zingine nyingi kwa watoto.

Kwa upande wake Ofisa wa masoko wa tigo, Benny  Lutaba, alipongeza kwa sherehe hiyo na kuomba jamii kuendelea kuwaunga mkono kwa bidhaa zao hapa nchini sambamba na kusaidia jamii kwa rika zote.

Nae Wenceslaus Kisarika ambae ni Marketing Manager wa K&K pamoja  Cons  Ltd  alipongeza kwa hatua ya watu kukumbuka watoto hasa waishio kwenye mazingira hatarishi na magumu hapa nchini.

“Tumefarijika sana kuunga kwenye siku hii muhimu, hakika jamii iiige mfano huu wa kuwakumbuka watoto hasa wanaohitaji msaada si utoe fedha hata kuwaleta mahala kama hapa ni moja ya kuwatimizia mahitaji yao” alisema Wence.

Aidham mbali na tigo,  American Garden kwa upande wao waliweza kuwa ‘surprise’ watoto  kwa kuwapatia zawadi za bidhaa zao zinazopatikana nchini kote.
 
Akizungumza na mtandao huu kwenye sherehe hiyo, Ofisa masoko wa Kingsway International (T) ltd,  American Garden, Miraji Chambuso  alipongeza kwa hatua hiyo ya kuwakumbuka watoto hao na ni moja ya kuhamasisha utalii wa ndani.

“Watoto wanapopata nafasi ya kufika sehemu kama hizi ni kuhasisha utalii wa ndani na sisi tupo mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wanatimiza ndoto na malengo yao” alisema Miraji.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages