Taswira Za Mkutano Wa CHADEMA Wilayani Same,Wazidi Kuvuna Wanachama Wapya Kutoka CCM na Katibu Mkuu wa Chama Cha TLP Same Ajiunga na Chadema - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Taswira Za Mkutano Wa CHADEMA Wilayani Same,Wazidi Kuvuna Wanachama Wapya Kutoka CCM na Katibu Mkuu wa Chama Cha TLP Same Ajiunga na Chadema

  James Ole Millya akihutubia
 Katibu Mkuu wa TLP Same, Heriel Msolo(kulia) akirudisha kadi jana Mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd Jhon Heche(wa pili kushoto)na Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema(Kushoto)
  Vijana wakigombea ofa ya kadi 10 za Millya
  James Ole Millya akisalimiana na mwanachama wa CCM aliahamia CHADEMA Same jana
  Aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini(CHADEMA), Godbless Lema akiwasili Same
  Wananchi wa Same wakigombea foleni ya kupatiwa kadi za CHADEMA jana
-- 
Habari na  Seria Tuma

CHADEMA wanaziara ya kichama Wilayani Same kwa siku nne,kuanzia jana hadi jumatatu chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana BAVICHA, Ngd John Heche.

Wana mikutano maeneo tofauti ya Wilaya katika kuimarisha chama hicho.Mkutano wa jana ulifanyikia viwanja vya Kwasakwasa Mjini Same kuanzia saa 9 hadi saa 12 jioni

Viongozi waliohudhuria ni pamoja na aliekuwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mwenyekiti Bavicha, John Heche, Mweyekiti CHADEMA Kilimanjaro, Augustino Matemu na kiongozi wa vijana Babati, Wilson Mattaka.

Wengine ni James Ole Millya aliekuwa Mwenyekiti UVCCM Arusha, aliekuwa Mjumbe wa NEC CCM kutoka Arusha, Ndg Ally Bananga na aliekuwa Diwani wa Sombetion (CCM). WOte hawa walihamia CHADEMA mapema mwezi huu

Katika mkutano huo kadi nyingi sana zilitolewa na kuasiniwa na John Heche..tena zikigombewa kununua. Lema litoa ofa ya kadi 10 kwa kina mama na Millya nae akatoa ofa ya kuwalipia vijana kumi..

Aliekuwa Katibu Mkuu wa TLP Same, Ndg Heriel Msolo alirudisha kadi ya TLP na kupewa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa BAVICHA, John Heche

Lema aliwataka watanzania kutokubali kugwanywa na wanasiasa kwa misingi ya udini na ukabila au ukanda na kueleza kwamba CHADEMA haipiganii maslahi ya kundi lolote katika hayo. Akasema hata yeye hapiganiimaslahi yake binafsi bali ya watanzania.

John Heche aliwataka watanzania kujitokeza kutoa maoni yao kwa tume ya Katiba na kuelekeza kuwa wakatae au wazifanyie mabadiliko makubwa nafasi za uDC au uRC na nyinginezo za kuteuliwa na mtu mmoja. Akadai pia madaraka ya rais ni makubwa na mamabo mengi yameachwa kwa mtu mmoja. hali inayohitaji marekebisho ili kuwe na uwajibikaji wa pamoja..

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages