KIJANA SHABANI ISSA APATIWA MATIBABU NA SASA ANAENDELEA VIZURI.SHUKRANI KWA WOTE WALIOSAIDIA KATIKA HILI.MUNGU AWAZIDISHIE PALE MLIPOTOA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

KIJANA SHABANI ISSA APATIWA MATIBABU NA SASA ANAENDELEA VIZURI.SHUKRANI KWA WOTE WALIOSAIDIA KATIKA HILI.MUNGU AWAZIDISHIE PALE MLIPOTOA

Mtoto Shabani Issa kabla hajaenda kufanyiwa upasuaji

Mnamo Tarehe 15 Mwezi wa 3 2012 Blogu ya Lukaza iliwahi kupost habari ya Kijana Shabani Issa ya kuomba msaada wa Kwenda kupata Matibabu  kutokana na hali yake ya Jicho kuwa na Uvimbe hivi sasa Kijana Shabani Issa anaendelea Vizuri baada ya Kupata matibabu katika Hospitali ya St Benedict Ndanda iliyopo Mkoani Mtwara.Kwa habari ya Kwanza ya Kijana Issa Kuomba Msaada  BOFYA HAPA
Kijana Shabani Issa Akiwa katika Hospitali ya St Benedict iliyopo Mkoani Mtwara baada ya kufanyiwa upasuaji.

Shabani Issa afanyiwa upasuaji jana(27/3/2012) St.Benedict's hospital Ndanda mkoani Mtwara.Anaendelea vizuri mpaka sasa.Namshukuru yeye aliyesimamisha mbingu bila kuweka nguzo kwa mema yake yote ktk shida ya kijana huyu.Nawashukuru wadau walioweza kuchangia kwa namna moja au nyingine.Najua wengine walijua ni uongo natafuta namna ya kuneemesha tumbo na wao nawashukuru pia.Naishukuru hospital ya Ndanda hasa dr.Mathew Ng'onye na Z.A Umbaro kwa jitihada zao ktk kufanikisha upsuaji salama.Mungu awabariki sana

Mtandao Wa Lukaza Blog Unapenda Kutoa shukrani Kwa Wadau Wote Waliowezesha Kijana Huyu Kupatiwa Msaada wa Kupata Matibabu Katika Hospitali ya Mtakatifu Benedict iliyopo Mtwara Mungu Awazidishie pale mlipotoa Kwa Kujali na Kuonyesha Upendo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages