Taswira Kutoka Mkutano Wa Tano Wa Mawaziri Wa Mamlaka Ya Ziwa Tanganyika Huko Kigoma - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Taswira Kutoka Mkutano Wa Tano Wa Mawaziri Wa Mamlaka Ya Ziwa Tanganyika Huko Kigoma

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma John Mogella akifunguwa Mkutano wa Tano wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika,kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mkutano huo umehusisha Nchi za Tanzania,Zambia,Burundi na Congo kwenye Hotel ya Lake Tanganyika
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Dk Terezya Huvisa akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika Bw. Dk Henry Mwima wakati wa Mkutano wa Tano wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika uliofanyika kwenye Hotel ya Lake Tanganyika Mkoani Kigoma
Mawaziri wa Nchi za Mamlaka ya Ziwa Tanganyika wakiangalia Ngoma [pichani haipo] wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika uliofanyika kwenye Hotel ya Lake Tanganyika Mkoani Kigoma.Picha na Ali Meja
---
Na Lulu Mussa-Kigoma

Mkutano wa Tano wa Mawaziri wa Mamlaka ya ziwa Tanganyika umefanyika leo mkoani Kigoma, ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya mkataba uliounda mamlaka hiyo.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dk. Terezya Huvisa amesema kuwa ili kulinusuru Ziwa Tanganyika jitahada za Nchi zote nne ni muhimu katika kukabiliana na changamoto zinazolikabili ziwa hilo kwa sasa kwa kutumia fursa zilizopo.

Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uchafuzi mkubwa wa mazingira ikiwa ni pamoja na kujaa kwa taka za majumbani na zile za viwandani, uvuvi haramu kutokana na ongezeko la watu, kilimo na ufugaji usio endelevu. Hata hivyo Waziri Huvisa amewakumbusha wajumbe wa Mkutano huo kuwa Ziwa Tanganyika linaunganisha Nchi zote nne badala ya kuzitenganisha, hivyo ni muhimu kuwa na mikakati endelevu ya kuhifadhi ziwa hilo.

Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa katika Mkutano huo ni pamoja na Utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kitaifa ambao kwa sasa unafanya kazi katika nchi zote pamoja na Mkakati wa kukusanya fedha kwa ajili ya kuwa na usimamizi endelevu wa Ziwa Tanganyika baadaya ya mwaka 2013 ambapo fedha za wafadhili zitafikia kikomo.

Katika Mkakati huo wa kukusanya fedha Nchi zote nne zimetia saini makubaliano ya kuchangia fedha ili hifadhi ya Ziwa hilo iwe endelevu, ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Mkutano huo umefanyika Tanzania kwa mara ya pili, mkutano mwingine kama huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwaka 2007. Mamlaka hiyo ya Ziwa Tanganyika inaundwa na nchi za Zambia, Burundi, Congo (DRC) na mwenyeji Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages