Baraza la Vijana wa CHADEMA Linakaribisha Maombi ya Kushiriki Mafunzo ya Wanasiasa Vijana Nchini Ujerumani Agosti 2012 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Baraza la Vijana wa CHADEMA Linakaribisha Maombi ya Kushiriki Mafunzo ya Wanasiasa Vijana Nchini Ujerumani Agosti 2012

Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) limekuwa na kawaida ya kutoa fursa za mafunzo ya makada wake ndani na nje ya Tanzania.

Dira ya BAVICHA ni kuona vijana ni nguvu ya mabadiliko ya kidemokrasia kwa maendeleo yao na ya taifa.
Kwa awamu hii BAVICHA limepanga kupeleka kada wake kwenye mafunzo ya wiki moja kwa wanasiasa vijana (Summer School) Berlin, nchini Ujerumani.

BAVICHA inawaalika vijana wa CHADEMA watakaopenda kushiriki mafunzo hayo kutuma barua ya maombi ya kushiriki, ikiambatana na wasifu unaojitosheleza (CV).

BAVICHA inahimiza vijana kutuma maombi kwa kuwa taarifa za waombaji zitahifadhiwa katika kumbukumbu (data bank) kwa ajili ya fursa nyingine zinazojitokeza.

Mwombaji pia anatakiwa ataje mawasiliano yake, namba ya kadi yake ya uanachama, tarehe ya kujiunga na chama na aeleze ushiriki wake ndani ya BAVICHA na Chama pamoja na matarajio yake ndani ya BAVICHA na CHADEMA kwa ujumla.

Maombi yatumwe kwa 
Katibu Mkuu wa BAVICHA kupitia
kabla ya tarehe 10/03/2012.

Dhima ya BAVICHA ni kuwezesha uwepo wa sera sahihi , uongozi bora na kujenga oganaizesheni thabiti ya vijana kwa maendeleo endelevu.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages