SPORTPESA KUWAFUTA MACHOZI WASHINDI WA TIKETI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

SPORTPESA KUWAFUTA MACHOZI WASHINDI WA TIKETI

Kampuni ya michezo ya kubashiri nchini ya SportPesa imekabidhi kiasi cha TZS 12,000,000/= kwa washindi 12 wa promosheni za Zali la Mwanaspoti na Shinda na SportPesa. Washindi hawa 12 walijishindia tiketi za kwenda nchini Uingereza kushuhudia mechi ya Ligi Kuu nchini humo kupitia promosheni za Zali la Mwanaspoti na Shinda na SportPesa lakini kutokana na sababu mbalimbali wameshindwa kusafiri hivyo kila mmoja wao kukabidhiwa TZS 1,000,000/= kama fidia ya safari hiyo.


Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti, SportPesa Tanzania Ndugu Tarimba Abbas alisema “Kampuni yetu ina ushirika na klabu mbalimbali ambapo endapo mshindi atapata nafasi ya kwenda kushuhudia mechi atapata nafasi ya kutembelea makao makuu ya klabu hizo ikiwemo Arsenal na Everton.



Kutokana na vigezo na masharti vya promosheni hizi mbili, hatutawaacha washindi wetu mikono mitupu bali kila mmoja wao ataondoka na kiasi cha shilingi milioni moja ambazo watazitumia wapendavyo, na hii ni kwa mujibu wa masharti ya promotion hizo.” Nae Ndugu Musa Yohana Tupa kwa niaba ya washindi wengine alisema



Kwanza kabisa napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa kampuni ya SportPesa, Mimi ni mshindi niliyepatikana kupitia promosheni ya Shinda na SportPesa. “Kutokana na shughuli zangu binafsi niliomba kutosafiri hivyo kuitaka kampuni inilipe fedha badala ya safari kama kanuni na masharti ya promosheni yanavyoelekeza.


No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages