Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti, SportPesa Tanzania Ndugu Tarimba Abbas alisema “Kampuni yetu ina ushirika na klabu mbalimbali ambapo endapo mshindi atapata nafasi ya kwenda kushuhudia mechi atapata nafasi ya kutembelea makao makuu ya klabu hizo ikiwemo Arsenal na Everton.
Kutokana na vigezo na masharti vya promosheni hizi mbili, hatutawaacha washindi wetu mikono mitupu bali kila mmoja wao ataondoka na kiasi cha shilingi milioni moja ambazo watazitumia wapendavyo, na hii ni kwa mujibu wa masharti ya promotion hizo.” Nae Ndugu Musa Yohana Tupa kwa niaba ya washindi wengine alisema
Kwanza kabisa napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa kampuni ya SportPesa, Mimi ni mshindi niliyepatikana kupitia promosheni ya Shinda na SportPesa. “Kutokana na shughuli zangu binafsi niliomba kutosafiri hivyo kuitaka kampuni inilipe fedha badala ya safari kama kanuni na masharti ya promosheni yanavyoelekeza.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)