Airtel Money Inasaidia WFP kutuma Pesa kwa Wakimbizi katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Airtel Money Inasaidia WFP kutuma Pesa kwa Wakimbizi katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu

Pichani ni Baadhi ya wakimbizi katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu wakipewa mafunzo toka kwa wafanyakazi wa Airtel huduma kwa wateja ya jinsi ya kutumia huduma ya Airtel Money tap tap card, kadi hiyo Inasaidia WFP kutuma Pesa kwa Wakimbizi katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu. Kadi ya Airtel Money Tap tap imeunganishwa na akaunti za Airtel Money ili kutoa usalama wa utumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya mtandao bila ya kuwa na simu ya mkononi. 

·        Kadi ya Airtel Money Tap Tap  inatumiwa na wakimbizi katika manunuzi ya bidhaa na kutoa hela
·        Huduma hii inatoa usalama wa utumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya mtandao bila ya kuwa na simu ya mkononi. 

Airtel Tanzania imeanzisha njia  mpya  na rahisi ya Near – Field Communication (NFC) ambayo ni mfumo wa malipo utakaoisaida Shirika la chakula Duniani  (WFP)  kuhamisha fedha kwa wakimbizi wapatao 10,000 kama sehemu ya mgao wao wa chakula kwa miezi mitatu ikiwa ni  mpango wa majaribio wa kuboresha huduma katika kambi ya wakimbizi ya  Nyarugusu.

Chini ya majaribio hayo, kwa sasa wakimbizi hao watapokea fedha kwa njia ya simu ya mkononi yenye dhamani ya  fedha za kimarekani $ 4.50 (shilingi 10,000) mara mbili kwa mwezi wakiwa katika kambi hiyo. Fedha hizo zitawekwa katika kadi zao za  Airtel Money Tap Tap kadi zilizounganishwa na teknolojia ya malipo ya NFC ambao umeunganishwa na akaunti zao za Airtel Money. Tap Tap kadi inatoa urahisi wa malipo na ni njia rahisi inayomfanya mteja kufanya malipo bila ya kuwa na simu yake ya mkononi  wakati wowote. Ni ufumbuzi  mzuri kwa wakimbizi  unaowawezesha kufanya shughuli za haraka na kwa urahisi kwa kugusisha tu kadi  kadi zilizounganishwa  na akaunti zao za Airtel Money na kufanya malipo ya kupokea au kununua bidhaa.

"Tap Tap  kadi imeungwanishwa na huduma ya Airtel Money ili inatoa huduma ya kipekee na urahisi kwa wateja wetu  katika utumiaji wa  wa fedha kwa njia ya mtandao, inawawezesha  wateja kutumia teknolojia ya kisasa kabisa yakufanya malipo au kuwa na uwezo wa kumiliki akaunti zao za fedha kwa njia ya mtandao hata kama simu ikiwa imezima," alisema Mkuu wa kitengo cha huduma cha  Airtel Money, Isack Nchunda. "Tunafura kubwa kuona kadi hizi mpya zinawawezesha  kufanya manunuzi ya chakula na kusaidia maisha ya wakimbizi waishio Tanzania."

Baada ya kupokea fedha kutoka kwenye kadi ya Tap Tap, wakimbizi wanauwezo wa kununua  chakula katika soko la Nyarugusu ambalo lilifunguliwa mwaka 2016. soko, hilo lipo maeneo ya buffer zone kati ya kambi na wenyeji wa maeneo hayo, ambapo imewapa nafasi  wafanyabiashara wa maeneo hayo kuweza  kuuza mazao yao kwa wakimbizi.

"Matumizi ya kadi hizo inawarahisishia wakimbizi kukidhi mahitaji yao ya chakula na wakati huo huo  kuinua uchumi wa nchi kwakuwa wanyeji hujipatia soko kwa bidhaa zao," alisema Mwakilishi wa WFP nchini Michael Dunford. "Pamoja na fursa kubwa ya kununua aina mbali mbali ya vyakula vinavyozalishwa ndani ya nchi na kuwasaidia kukidhi malazi, vilevile inasaidia kuboresha hali ya lishe ya kaya na kuhakikisha kwamba jamii na wenyeji pia wanafaidika kupitia shughuli nyingi za kiuchumi."

Katika kipindi hiki cha majaribio , wakimbizi wataendelea kupokea mafuta, uji na vitu vingine vidogo wakati mgawo wa wa nafaka, kunde na chumvi vitabadilishwa kwa fedha taslimu.alisisitiza Dunford

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages