Jinsi Teknologia ilivyo rahisisha zaidi utafutaji wa ajira Tanzania - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Jinsi Teknologia ilivyo rahisisha zaidi utafutaji wa ajira Tanzania

Miaka 10 iliyopita secta ya ajira ilikuwa tofauti sana na ilivyo leo hii, utaftaji wa ajira ulikuwa ni tofauti sana na ilivyo hivi sasa. Matangazo ya ajira yalikuwa yakitegemea zaidi magazeti na serikali kufikia hatua ya kufanya ni lazima kila kampuni binafsi na hata mashirika ya uma kutangaza ajira mpya kupitia kwenye kurasa za magazeti.

Wengi wetu tuna fahamu kuwa magazeti kama vile Daily News, Mwananchi, The Guardian pamoja na The citizen ndiyo magazeti maarufu sana katika kutangaza matangazo ya ajira.

Magazeti haya ambayo huchapishwa kila siku yamekuwa msaada mkubwa sana kwa wale wanao tafuta ajira na sehemu kuu ya kusoma ajira mpya zinazotangazwa kila kukicha basi ni kwenye kurasa za magazeti haya.

Mabadiliko ya tekinologia yamekuja kimageuzi kwenye secta hii na kuongeza urahisi zaidi kwa watafutaji wa ajira hapa nchini Tanzania. Kuanzia mwaka 2007 ndipo mabadiliko haya yalipo anza kuibuka baada ya tovuti mbali mbali zinazotoa matangazo ya jira mitandaoni kuibuka kwa kasi zaidi.

Ukuaji huu wa mitandao ya matangazo ya ajira imeleta mabadiliko ambayo leo hii imekuwa ni faida sana kwa pande zote mbili mbazo ni watafuta wa ajira na waajiri.

Asilimia 80 ya makampuni yanayo jishughulisha na kutafutia waajiri wafanya kazi, wengi wetu tukiyafahamu kwa lugha ya kigeni “Recruitment Agencies” wana weka matangazo yao kwenye mitandao.

Tovuti kama vile Jobstanzania nao pia wameongeza wigo na kurahisisha zaidi huduma hii kwa kuanzisha tovuti inayo toa taarifa za matangazo ya ajira kila siku. Ambapo pia wana toa fursa kwa waajiri kuweka matangazo ya ajira kwenye mtandao bure kabisa.

Achilia mbali urahisi huu wa kupatikana kwa matangazo ya ajira, hivi sasa tekinologia pia imerahisisha hata pia njia za uombaji kwa wanao tafuta ajira. Hapo awali njia kuu yakutuma maombi ya ajira ilikuwa ni kupitia posta lakini leo hii kuna mabadiliko makubwa sana ikiwa waombaji wa ajira wanaweza kutuma maombi kwa barua pepe (Email) na kumfikia mwajiri kwa haraka zaidi.

Japokuwa tatizo la ajira kwa vijana wanao hitimu chuo kwa sasa limezidi kuwa kubwa, hii ni kiashirio kuwa sasa vijana wanajiendeleza kielimu lakini tatizo ni ajira. Serikali inajitahidi sana kupunguza wimbi la vijana wasio na ajira lakini bado kuna uhaba wa ajira.

Suluhisho ni nini?
Unaweza jiuliza je ni vijana wangapi wana hitimu kwenye vyuo vikuu vyetu hapa Tanzania? Jibu ni maelfu na hawa wote wanahitaji ajira wakati huo huo ajira bado ni chache sana.

Nini Kifanyike?

Ajira sio suluhisho, kuna fursa nyingi sana kwa vijana kufanya na kujikwamua kiajira kwa kujiajiri wenyewe. Naamini katika vyuo vyetu vina fundisha somo la ujasiliamali (Entrepreneurship), basi kama vijana wanao hitimu vyuo wakitilia maanani somo hili na kutafuta fursa za wao kujiajiri naamini janga la ukosefu wa ajira litakuwa na kikomo.

Je! wewe una mtazamo gani? toa maoni yako kupitia kwenye sehemu ya kutoa maoni hapa chini.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages