Naungana na Wewe Kupinga Vitendo vya kikatili juu ya Albino - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Naungana na Wewe Kupinga Vitendo vya kikatili juu ya Albino

"Ni kweli mimi ni Albino, nimejikubali na nimeishi maisha yangu yote bila kujali nilivyo. Sijawahi kutumia hali yangu kupata kitu kwa huruma, nimeyapigania maisha yangu na nimepiga hatua.

Leo hii naongea nanyi nikiwa Baba, Mume, Mwandishi Mwandamizi, Blogger, na mengine mengi, lakini hali yangu sasa inaanza kunikwaza.

Haya mauaji jamani, nimejiteua kuwa Balozi, nitatetea, na kusimama mbele ya wenzangu wote wenye hali kama hii, kama ni wanasiasa ama wafanyabiashara, wanataka kutuua kwa maslahi binafsi, mwaka huu HAPANA.

Wanaoniunga mkono mikono juu" Mwisho wa kunukuu.

Nikiwa kama Blogger na Mwanahabari Mwenza wa rafiki yangu na Kaka yangu Kipenzi,Henry Mdimu aliejitolea kuwa Balozi,nanyoosha mkono juu kwa kuunga mkono kupiga vita vikali mauaji ya ndugu zetu wenye Albinism.kwani wao pia ni Binadamu kama tulivyo mimi na wewe.
 
FATHER KIDEVU BLOG NA UONGOZI WAKE WOTE UKIONGOZWA NA MROKI MROKI 'FATHER KIDEVU' UMENYANYUA MIKONO JUU KUUNGANA NAWE ZEE LA NYETI.
 
JAMANI SASA BASI,NA KILA MMOJA WETU AWE MLINZI KWA NDUGU ZETU HAO.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages