FILAMU YA C.P.U IPO SOKONI SASA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

FILAMU YA C.P.U IPO SOKONI SASA

FILAMU kubwa ya C.P.U Kitengo cha kutetea Watoto imeingia leo sokoni kwa njia ya mtandao, lengo likiwa ni kuwafikia watu wengi Ulimwenguni, hivyo kwa utaratibu wa kampuni ya usambazaji ya Proin Promotions ni kuuza katika mtandao baadae katika Dvd na njia nyingine.


Leo Jumatatu tarehe 16.February. 2015 inapatikana mtandaoni unaweza kununua filamu hiyo kwa kutembelea www.proinpromotions.co.tz na kununua filamu ya C.P.U na filamu zingine za Proin Promotions utanunua na kuangalia full HD.

Sinema ya C.P.U imeshirikisha wasanii zaidi ya 230 huku wasanii wakongwe wenye majina kama Kulwa Kikumba ‘Dude’ Dotnata, Richard Mshanga ‘Mzee Masinde’, Hashim Kambi ‘Ramsey’, Sauda Simba, Subira Wahure, steve Sandhu, Nkwabi Juma, Mohamed Funga funga ‘Mzee Jengua’ Mobby Mpambala wakiwa vinara wa sinema hiyo.

C.P.U sinema ya kimataifa wiki ya pili itapatikana katika Dvd na kupatikana nchi nzima kutokana na mfumo mpya wa Proin Promotions kuuza kwa njia ya mtandao na wiki inayofuata utaweza kununua katika Dvd, NUNUA NAKALA YAKO HALALI YA C.P.U SASA!

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages