Kampuni ya Murhandziwa yakabidhiwa leseni ya Kuendesha Bahati nasibu ya Taifa - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Kampuni ya Murhandziwa yakabidhiwa leseni ya Kuendesha Bahati nasibu ya Taifa

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Michezo ya bahati nasibu , Bw Abbass Talimba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kukabidhi leseni ya kuendesha bahati nasibu ya Taifa kwa Kampuni ya Murhandziwa.
Mkurugenzi wa Bodi ya Michezo ya bahati nasibu, Abbass Talimba (kushoto) akikabidhi leseni kwa VIongozi wa Kampuni ya Murhandziwa ambao ndio wamepewa kibali cha kuendesha bahati nasibu ya Taifa nchini Tanzania.Aliyeshika Leseni hiyo ni Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Murhandziwa, Lucien D Avece.
Baadhi ya viongozi wa Kampuni ya Murhandziwa pamoja na viongozi wa Bodi ya Michezo ya Bahati nasibu ya Taifa
 Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika katika hoteli ya Double Tree by Hilton - Masaki.Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

TAARIFA YA PROF BONGANI AUG KHUMALO (MWENYEKITI WA GIDANI INTERNATIONAL (PROPRIETARY)LIMITED NA MURHANDZIWA LIMITED KATIKA HAFLA YA KUPOKE LESENI YA KUENDESHA SHUGHULI ZAKE NCHINI KUTOKA TAASISI  YA SERIKALI  INAYOSIMAMIA MICHEZO YA KUBAHATISHA NCHINI TANZANIA (2 FEBRUARY 2015, DAR ES SALAAM, TANZANIA)
  
Leo tunashuhudia ujio wa kampuni ya pili kwa ukubwa barani Africa  inayojishughulisha na michezo ya kubahatisha ikitangaza kuanza kutoa huduma zake hapa nchini.

Ujio wa kampuni hii  unategemewa kuleta manufaa kwa  nchi ya Tanzania na watanzania kwa ujumla waliopo katika sekta rasmi na  waliopo katika sekta zisizo rasmi yaani wafanyabiashara  binafsi.Shughuli zitakazofanywa na kampuni hii zitaingiza fedha nyingi za kigeni kwa serikali ambazo tuna imani zitatumika kuboresha maendeleo ya nchi na huduma kwa wananchi wake.

Kampuni ya Murhandziwa  mbali na kunufaisha wananchi kupitia mapato yatakayolipwa serikalini pia itatoa ajira kwa watanzania wengi na wengine wengi watanufaika kwa kufanya biashara  na kampuni hii kwa kutoa huduma na kuiuzia mahitaji mbalimbali.

Tutaanzisha maduka mbalimbali ambayo yatakuwa  yanaendesha michezo mbalimbali ya kubahatisha na  ambayo pia  yatakuwa yanauza tiketi za kushiriki kwenye michezo ya kubahatisha tutakayokuwa tunaendesha na tumejipanga kutokana na uzoefu wetu kuhakikisha tunaboresha huduma hizi kama ilivyo katika nchi mbalimbali duniani na kuthibitisha kwamba sekta hii ni moja ya sekta inayoweza kuchangia pato la taifa na kukuza uchumi kwa kiasi kikubwa.

Kampuni ya  Gidani International (Proprietary) Limited ambayo ni kampuni mama ya kampuni ya Murhandziwa Limited ili kuendesha  shughuli zake kwa ufanisi  nchini imejipanga kuwapatia ujuzi wa aina mbalimbali watanzania itakaowapatia ajira kuhusiana na fani ya michezo ya kubahatisha ambao yatatolewa na wataalamu  waliobobea katika fani hii kutoka nchi mbalimbali duniani.

Vilevile kampuni hii inatarajia  kuwa katika kipindi chote itakachokuwa inatoa huduma nchini itawawezesha watanzania wataoshiriki michezo mbalimbali itakayoiendesha kuwa mamilionea na imejizatiti kutoa huduma bora kwa washindi na washiriki wa michezo itakayokuwa inaendesha ikiwemo kuwashauri jinsi ya kufanya  uwekezaji wa busara kwa fedha watakazojishindia.

Kampuni ya Gidani International siku zote itakazokuwa inatoa huduma nchini itakuwa makini kuzingatia sheria za Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania na sheria elekezi kutoka Bodi ya Serikali ya kusimamia michezo ya kubahatisha ambayo iko kwaajili ya kuhakikisha michezo hii ya kubahatisha inaendeshwa kwa misingi ya sheria,usawa na bila udanganyifu wowote.

Tunaamini kuwepo kwa michezo hii kuwa ni moja ya sekta inayoshiriki katika  kukuza uchumi wa nchi na kupambana na  janga la kuondoa tatizo la umaskini kwenye jamii,na ndio maana serikali imekuwa ikitoa kibali cha kufanyiika michezo hii na ina bodi inayoratibu uendeshwaji wake nasi tukiwa wadau tutafanya kazi kwa karibu na serikali na vyombo vyake  ikiwemo  wananchi wa Tanzania ambao watakuwa wadau wakubwa wa michezo hii.

Tumefurahi kuja hapa nchi tukijua uhusiano mkubwa uliopo baina na Tanzania na Afrika ya Kusini katika Nyanja mbalimbali na tunaamini ujio wetu unazidi kuimarisha ushirikiano wa kibiashara baina ya nchi hizi mbili,kuzidi kuimarisha pia Muungano wa nchi za Afrika.Kwa kuzingatia hilo tutaheshimu sheria zote za nchi na kuendesha shughuli zetu kwa umakini na weredi mkubwa na kuhakikisha zinaleta manufaa kwetu sote.

Sekta ya michezo ya kubahatisha nchini itabadilika kwa muda mfupi na kutambulika barani afrika kutokana na uwekezaji wa kiteknolojia tutakaoufanya.Tunajivua kuwa  miundombinu na vifaa vyetu vya kuendesha michezo hii ni vya kiwango cha juu vilivyotengenezwa hapa hapa barani Afrika.Vituo 4,000 vya michezo na mauzo ya tiketi na  vifaa vingine vya kisasa vinavyohamishika zaidi ya 1,000 vitaletwa  hapa nchini hivi karibuni kwa ajili ya kuzindua huduma zetu.Tutaanza kuuza tiketi Julai 4 ambapo ndipo utafanyika uzinduzi rasmi.

Neno murhandiwa ni la lugha ya Tsonga moja ya lugha kubwa katika ya lugha 11 zinatotumiwa na watu wengi nchini Afrika ya Kusini likiwa na maana ya “Mpendwa wako”.Nina imani kubwa kuwa Murhandziwa itapendwa katika kila familia na wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla.

Mwisho

Imetolewa na Prof Bongani Aug Khumalo
Mwenyekiti
Gidani International (Proprietary) Limited
Murhandziwa Limited
Aggrey & Clifford 

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages