
Winga Mholanzi Anayepaa: Nyota wa Bayern, Arjen Robben amekuwa akishutumiwa kwa kujiangusha kirahisi
Angalizo
la tahadhari: Kocha wa Manchester United, David Moyes anatumai refa
Carlos Velasco Carballo atwaadhibu wachezaji wa kujiangusha.
KOCHA Mkuu wa Mashetani wekundu, Manchester United, David Moyes amemuambia mwamuzi wa Hispania, Carlos Carballo kutoa maamuzi sahihi katika mchezo wao dhidi ya mabingwa wa Ulaya na Bundesliga, Bayern Munich kutokana na tabia ya wachezaji wa timu hiyo kujiangusha.
Man United inakabilina na Bayern usiku wa leo uwanja wa Old Trafford katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali, Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bayern inapewa nafasi kubwa ya kushinda, lakini timu hiyo ya kocha Pep Guardiola ilishutumiwa baada ya kuitoa Arsenal katika raundi iliyopita, huku kocha wa washika bunduki wa London, Arsene Wenger akimlaumu Arjen Robben kuwa ni hodari wa kujirusha kujiangusha.
Moyes alisema: “Tunawaamini marefa watafanya uamuzi sahihi. Kujirusha ni moja ya vitu vibaya vya kufanyia kazi. Ningependa kutahadharisha juu ya hilo, lakini nisingependa kumlenga mchezaji binafsi,”.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA CHINI





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)