UTANGULIZI:
NETWORK ni moja ya filamu ya kitanzania iliyotengenezwa na
Na Kampuni ya Kalage Pictures ambayo ipo chini ya Mkurugenzi wake John Kalage lakini Pia ikiwa inatoka Swahilihood.
Ni moja ya Filamu inayouzwa na kusambazwa na kampuni ya
Proin Promotions Limited ambapo Kwanza Inapatikana
Kwenye Maduka Yote ya Kuuzia Filamu Nchini.
IFUATAYO NI MTAZAMO JUU YA UHALISIA WA FILAMU HIYO NA
MAZINGIRA YA KITANZANIA:
Kwanza Kabisa Filamu hii ina uhalisia kwa Asilimia 90 ambapo
kwa baadhi ya matukio yaliyomo kama Vile kulipiza Kisasi, Mauaji, Kuambukizwa
Kwa Makusudi magonjwa ya Zinaa nk ni baadhi ya matukio tu yaliyopo katika
Filamu hiyo, kiukweli matukio hayo yapo na yanatokea katika mazingira yetu tena
sana tu na Kiuhalisia Kweli hii filamu ina uhalisia na sio Filamu ambayo ina
matukio ya kusadikika.
JUU YA MCHANGANYIKO WA RANGI:
Kwanza kabisa nawapongeze Kalage Pictures kwa jinsi
walivyoweza kujitahidi sana katika zoezi zima la Kutengeneza filamu hii na
kuweza kuchanganya rangi vizuri na kupelekea kama Filamu hii ilitengenezwa kwa
Kutumia Kamera za zamani ambazo ndio zinatoa rangi kama hii, kiukweli ni rangi
ambazo unaweza kuzipata kwenye filamu za Zamani kutoka Hollywood yaani 1980s
kwa hilo kajitahidi sana. Na Rangi zake ni Nzuri pia na zinavutia.
JUU YA WAHUSIKA:
Kwanza kabisa katika filamu hii Muhusika Mkuu ni Ni
Muigizaji Mmoja aitwaye BRIAN IBRICK jina la kisanii alilotumia kwenye filamu
hii anaitwa Detective (Mpelelezi) Demango, Huku akisaidiwa na VYONE CHERRIE
wakati kwenye filamu hii anatumia jina la Detective Eliza (Monalisa huyo).
Hawa kweli waliweza kuuvaa uhusika haswa katika vipengele
walivyoigiza kwanza Nimuongelee Detective Eliza kiukweli aliuvaa uhusika haswa
pale katika kipengele cha kumkimbiza Kijana aliyekuwa akifanya biashara za
magendo hadharani na walipomkimbiza kweli Detective Eliza Aliweza kuonekana
akikimbia haswa pamoja na kutumia teknolojia kumuongezea mwendo lakini sehemu
kubwa aliweza kukimbia na kuonyesha kuwa alikuwa fit kwenye kipande kile na
jinsi alivyoweza kuigiza kama Mpelelezi
Nirudi kwa Mpelelezi Demango huyu yeye aliweza kabisa katika
Kuonyesha Jinsi gani watu wanaweza kuwaambukiza wanawake kwa makusudi kabisa
virusi vya ukimwi, na Vilevile kwa nafasi yake yeye kama Mpelelezi aliweza
kuonekana ni mmoja wa Wapepelezi wenye uzoefu wa siku nyingi lakini
aliyeshindwa kupata taarifa sahihi za Uhalifu mbalimbali wa mauaji yaliyoyokuwa
yakitokea na wizi kwasababu ya kupokea rushwa na Haya yapo Kwenye jamii
zetu....
Kiukweli waliweza kuuvaa uhusika haswa na kufanya filamu hii
kuonekana yenye uhalisia zaidi kuliko matukio ya kusadikika.
JUU YA UTOFAUTI NA FILAMU NYINGINE ZA KITANZANIA:
Kwanza utofauti wake mkubwa ni Kuanzia rangi zilizotumika,
zimetumika vizuri sana tofauti na filamu nyingine kuwa rangi zinakuwa
zimechanganywa kama mtu amelazimishwa, Pili filamu hii imetengenezwa takriba
miezi miwili tofauti na filamu nyingine zinatengenezwa ndani ya wiki kadhaa tu.
Tofauti nyingine ni Sauti Kwenye sauti zinasikika vizuri kabisa japokuwa Kuna
baadhi ya Matukio wameshindwa kuacha sauti halisi Mfano Mpelelezi Demango wakati anaongea na simu
huku akiendesha gari nilitarajia Kusikai Mlio halisi wa gari japo kwa mbali
ilikuweza kuleta uhalisia wa tukio hilo.Vipo vingi sana vinavyoonyesha Utofauti
na filamu nyingine.
JUU YA MFANANO NA FILAMU NYINGINE ZA KITANZANIA:
Hakika nimeshindwa kuelewa Kuwa Tasnia hii ya filamu
Tanzania wameshindwa kabisa kutofautisha Muundo wa FIlamu zao maana Stori huwa
nzuri lakini Sasa Unapoangalia Kipande kimoja unaweza kutabiri kipande kijacho
baada ya kuona kipande cha Nyuma na Kikawa kama ulivyoweza kutabiri , Filamiu
nyingi za Kitanzania unajua kabisa kinachofuata baada ya kipande hiki ni hiki
"ABCD". Kwa hili Badilikeni Bongo Movie.
JUU YA MAPUNGUFU YA FILAMU HII:
Kama ilivyo ukweli usiopingika kuwa Sisi Binadamu
hatujakamilika na Hakuna Kizuri kisicho na kasoro, Kasoro ni sehemu ya Maisha
yetu lakini Kwa Asilimia Kubwa Kasoro niliyoweza kuziona ni Kama Vile kwenye
kipande cha Mpelelezi Eliza alipokuwa akimuhoji Yule Kijana Ndani wakati
wakiwaonyesha kwa Karibu wakiweza kuonyesha kabisa Kuwa Kulikuwa ni Usiku na
Pembeni kulikuwa na giza lakini walishindwa kukumbuka kama waliweka Giza
matokeo yake kipande hiko wakikionyesha kwa Umbali kidogo panaonyesha Chumba
hiko kina Mwanga baadhi ya sehemu wakati mwanzo kulikuwa na giza.Kwa Hili rekebisheni
kwenye movie nyingine msirudie kosa kama hilo,maana wengine huwa tunaangalia
kwa umakini kama nini. Mapungufu mengine ni Kama Vile hatukuweza kusikia sauti
halisi badala yake walipandishia sauti japokuwa walifanya vizuri sana
kupandishia sauti na hawakuaribu kwasababu midomo na matamshi vilikuwa
vinaendana haswa kwa hilo Big Up. Hayo ni Baadhi tu
HITIMISHO
Kwa asilimia 90 Ni filamu nzuri sana Hasa kabisa ikiwa
inahakisi jina la Filamu na Matukio yaliyomo humo na vilevile ni filamu
inayosisimua na Kuelezea Visa halisi kabisa vinavyotokea katika Jamii zetu
zinazotuzunguka.
Pongezi kwa John Riber kwa Kusupport tasnia hii ya filamu na
kuleta mabadiliko katika Tasnia hii ya Filamu Tanzania. Vilevile Pongezi kwa
Kalage kwa kuweza kuitengeneza Filamu Hii haswa katika viwango vingine vya Juu
zaidi, Mapungufu yapo lakini tuyafanyie kazi ili Kuweza kutoa kazi nzuri hapo
baadae.
Shukrani kwa Proin Promotions Limited kwa Kusambaza filamu
hii nchini.na Kuamua Kupokea kazi bora kabisa.
JIPATIE NAKALA YAKO SASA....





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)