MDAU GLADNESS NKYA ASHEHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA JIJINI MWANZA. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MDAU GLADNESS NKYA ASHEHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUTOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA JIJINI MWANZA.

 Bi. Gladness Nkya akikabidhi zawadi kwa wawakilishi wa Kituo cha Upendo Daima katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake ambapo badala ya kufanya sherehe ya kunywa na kula pamoja na marafiki ameamua kwenda kusheherekea na watoto yatima katika kituo hicho.
 Gladness Nkya akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa kituo cha watoto yatima cha Upendo Daima.
Baadhi ya marafiki wa Bi. Gladness Nkya wakiwa katika picha ya pamoja walipomsindikkiza rafiki yao Gladness Nkya kwenda kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa na watoto yatima. 

Imekuwa hali ya kawaida kwa watu mbalimbali hasa vijana kusheherekea siku ya kuzaliwa kwa hafla mbalimbali pamoja na marafiki ambapo hunywa vinywaji mbalimbali na kula vyakula wakati mwengine mpaka kusaza lakini hilo limekuwa tofauti kwa mdau Gladness Nkya ambae yeye ameona atue fursa ya siku hiyo kusheherekea pamoja na watoto yatima wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Upendo Daima kilichopo Nyegezi, Malimbe karibu kabisa na Chuo Kikuu cha Mt. Augustino jijini Mwanza.

Unaweza kuona ni vitu vidogo lakini moyo mkubwa aliokuwa nao Bi. Gladness katika kusaidia wengine wenye mahitaji Zaidi yake ni kitu cha kuigwa na cha mfano kwa vijana wengine ambao wana nafasi ya kuisadia jamii inayowazunguka. Wahenga walisema “Kutoa ni Moyo na si utajiri”.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages