SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUENDELEZA MCHEZO WA RIADHA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUENDELEZA MCHEZO WA RIADHA

IMG_8774
Mkurugenzi wa Purosangue Athletic Club, Bw. Nico Angelo Pannevis (kushoto) akimweleza jambo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel alipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumueleza mpango wa Klabu yake kushirikiana na Tanzania Kuwaendeleza Wanariadha chipukizi nchini.IMG_8784Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel  akisisitiza jambo wakati akizungumza na Mkurugenzi wa Purosangue Athletic Club, Bw. Nico Angelo Pannevis (katikati) alipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumueleza mpango wa Klabu yake kushirikiana na Tanzania Kuwaendeleza Wanariadha chipukizi nchini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Bw. Leonard Thadeo.
IMG_8797Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel (kushoto) na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Bw. Leonard Thadeo (kulia) wakionyeshwa tisheti yenye logo ya Klabu ya Purosangue Athletic ya nchini Italia leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Klabu hiyo, Bw. Nico Angelo Pannevis. Klabu hiyo imeonyesha nia ya kuendeleza vipaji vya Wanariadha chipukizi nchini kwa kujenga kituo kwa ajili ya mpango huo. Picha na Concilia Niyibitanga,
………………………………………………………………
Na Genofieva Matemu,
              Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
         Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
     Serikali ya Tanzania kushirikiana na Wadau wa mchezo wa Riadha kuinua vipaji
Serikali ya Tanzania kwa kushirikana na wadau wa mchezo wa riadha kutoka  nchini Italia imepania kuendeleza mchezo wa riadha  ili kuinua vipaji vya wanariadha chipukizi nchini.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel wakati akiongea na Mkurugenzi wa Klabu ya Purosague Athelics  ya Italia, Bw. Nico Angelo Pannevis alipomtembelea ofisini kwake.
Prof Gabriel amesema kuwa Serikali iko tayari kushirikiana na Wadau wa Mchezo wa Riadha ili kuhakikisha kuwa Wanamichezo chipukizi wanaendelezwa na kufanya vizuri katika mashindano ya Kitaifa na Kimataifa.
Naye Bw.Pannevis ameeleza mpango wa Klabu yake wa kujenga kituo cha Mchezo wa Riadha hapa nchini ili kuwaendeleza Wanariadha chipukizi katika kuwajengea uwezo katika mchezo huo na fani nyingine za maisha.
Aidha, Bw. Pannevis amesema kuwa hapo baadae Klabu yake haitajikita tu kwenye riadha bali pia inalenga kuendeleza michezo ya walemavu ili kuwawezesha kufikia ndoto zao za kimichezo kama wanamichezo wengine.
Alikiri kuwa Klabu yake imechagua kuendeleza michezo Tanzania ili kuitangaza Tanzania kupitia mashindano mbalimbali ya michezo ya Kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages