THOMAS MASHALI AWAFANANISHA MADA MAUGO NA KALAMA NYILAWILA KAMA MIDOLI WAKE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

THOMAS MASHALI AWAFANANISHA MADA MAUGO NA KALAMA NYILAWILA KAMA MIDOLI WAKE

IMG_7213 Bondia Thomas Mashali akionesha midoli yake anayoifananisha na mabondia wenzake, Kalama Nyilawila (kushoto) na Mada Maugo, wakati wa mazoezi yake yanayoendelea katika gym yake iliyopo Manzese, Dar es Salaam IMG_7201
Bondia Thomas Mashal
 
Hatua hiyo ya Mashali inatokana na awali kupondwa na Maugo kuwa hana uwezo na ni heri akageukia biashara ya kuuza chapati, wakati Kalama akimkebehi kuwa ni kibonde wake.Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili katika gym yake, Manzese, Dar es Salaam jana, Mashali alisema mabondia hao hawana uwezo wa kupambana naye kwa sasa na ni kama midoli kwake.
 
Mashali, ambaye atapanda ulingoni Oktoba 30 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee kuzichapa na Maugo, yuko katika mazoezi makali kwa ajili ya pambano hilo kabla ya baadaye kupigana na Nyilawila.

“Unajua hawa ni kama midoli kwangu (huku akionesha midoli aliyoshika), na kwa kudhihirisha hilo nitaanza na maugo Oktoba 30 kumuonesha kuwa hatakiwi kuzungumza asichokijua,” alisema Mashali.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages