MANCHESTER UNITED YAUA 5-2, WELBECK, LINGARD WAMETUPIA KAMA KAWAIDA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

MANCHESTER UNITED YAUA 5-2, WELBECK, LINGARD WAMETUPIA KAMA KAWAIDA

.com/blogger_img_proxy/Mashabiki wapatao  40,000-walijitokeza uwanja wa Hong Kong  kuitazaman mechi hiyo
.com/blogger_img_proxy/Safi kijana: Tom Cleverley na Anderson wakimpongeza  Fabio baada ya kuifungia United bao la tatu 
.com/blogger_img_proxy/Risasi: Lam Ka Wai (wa pili kulia) akishangilia bao la kwanza la kusawazisha na kufanya ubao wa matangazo kusomeka 4-1
.com/blogger_img_proxy/Bao la kwanza: Danny Welbeck akishangila bao lake la kwanza katika ushindi wa leo
.com/blogger_img_proxy/Hapa rangi nyekundu tu: Uwanja wa Hong Kong  ulijaza mashabiki wengi ambao lengo lao lilikuwa kuwashuhudia wakali wa soka la England
.com/blogger_img_proxy/
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com

Mabingwa wa ligi kuu soka nchini England, Manchester United wamecheza mechi yao ya tano katika ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi dhidi ya  Kitchee ndani ya uwanja wa  Hong Kong  na kuibuka na ushindi wa mabao 5-2.

Mechi ya leo ilitakiwa kuchezwa mwishoni mwa wiki iliyopita, lakini Kocha wa United, David Moyes alilazimika kuahirisha mechi kwa madai kuwa uwanja wa Hong Kong ulikuwa mbovu kufuatia mvua kunyesha na uwanja kujaa matope, huku ukiwa umetumika mfululizo katika michuano ya kombe la  Barclays la Asia.

Hali ya uwanja siku ya jumamosi wakati wa fainali ya Sunderland na Manchester City ilikuwa mbaya sana, lakini viongozi walijitahidi kufanya jitihada za kurekebisha kabla ya mchezo wa leo. Kikosi cha Kitchee: Comi, Rodriguez, Rehman, Kei, Alkande, Belencoso, Wai, Annan, Yang, To.

Wachezaji wa akiba: Jianqiao, Wen, To, Fung, Quankun, Hau, Fai, Paramo, Lam, Deshuai, Lung

Waliofunga Magoli yao: Lam (53), Alkande (69)

Kikosi cha Manchester United: Amos, Evra (Buttner HT), Anderson, Smalling, Carrick (Jones 72), Young (Januzaj HT), Welbeck (Lingard HT), Fabio (Rafael 72), Cleverley, Zaha, Keane.
Wachezaji wa Akiba: Lindegaard, Rafael, Jones, Ferdinand, Giggs, Van Persie, Buttner, Lingard, Januzaj.

Waliofunga mabao: Welbeck (16), Smalling (22), Fabio (26), Januzaj (47), Lingard (80)

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages