Kocha Wa Man United Sir Alex Ferguson akiwa amemshikilia mwali Baada ya Kukabidhiwa Mwali leo baada ya kuichapa Swansea magoli 2 kwa 1 na kumaliza ligi kuu ya Uingereza Vizuri
Sir Alex Ferguson ambaye hivi karibu ametangaza kustaafu kuifundisha Man U akifurahi kombe na wachezaji wa Man United mara baada ya kukabidhiwa kombe leo.
Sir Alex Ferguson akinyanyua juu kombe la ligi kuu ambalo amelichukua katika msimu wake wa mwisho wa ligi kuu ya uingereza na huu ndio msimu wa Mwisho na Kombe la Mwisho kwa Sir Alex Ferguson
Wayne Rooney Akishangilia huku amenyanyua Kikombe Cha Ligi Kuu ya Uingereza mara baada ya kukabidhiwa kombe lao leo
Kikosi Cha Man U kikishangilia Kwa Shangwe za Kutosha Mara baada ya Kukabidhiwa Kombe lao
Sir Alex Ferguson akiwaaga mashabiki wa Man U na wadau wa soka waliojitokeza kushuhudia mtanange wa Man U na Swasea ambapo Man U imemaliza ligi Vizuri kwa kuitungua Swasea Magoli 2 kwa 1 na hatimaye kukabidhiwa Kombe lao
Alama za Nyakati: Shabiki wa Man U akionyesha Jinsi Jina la Kocha Sir Alex Ferguson lilivyonyambuliwa na kutoa maana kama ambavyo linaonekana kwenye picha
Paul Scholes akishangilia na kushukuru kwa mechi ya leo ambayo ndio Mechi yake ya Mwisho kucheza akiwa na Man U huku akitangaza Kustaafu kucheza soka.Picha Kwa Hisani ya Mtandao
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)