China yahimizwa kuwekeza sekta ya Utalii nchini Tanzania - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

China yahimizwa kuwekeza sekta ya Utalii nchini Tanzania

Ujumbe kutoka Tanzania na Maofisa wa Kamisheni ya Utalii ya Chaoyang, Beijing katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo ya kutUjumbe kutoka Tanzania na Maofisa wa Kamisheni ya Utalii ya Chaoyang, Beijing katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo hayo. Ujumbe kutoka Tanzania ukiwa katika mazungumzo na Maofisa wa Kamisheni ya Utalii kutoka Chaoyang, Beijing yenye lengo la kutangUjumbe kutoka Tanzania ukiwa katika mazungumzo na Maofisa wa Kamisheni ya Utalii kutoka Chaoyang, Beijing yenye lengo la kutangaza utalii wa Tanzania.
………………………………………………………………
Na Pascal Shelutete, Beijing

Tanzania imehimiza wawekezaji kutoka China kuwekeza katika sekta ya utalii ambayo ina fursa nyingi ambazo bado hazijatumiwa ipasavyo. Mkurugenzi wa Utalii  kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Ibrahim Mussa alisema hayo jana alipokutana na ujumbe Kamisheni ya Utalii ya Chaoyang jijini Beijing  nchini China.

Bw. Mussa ambaye anaongoza ujumbe kutoka Tanzania unaotembelea China kwa lengo la kutangaza utalii wa nchi yetu alisema kuwa Tanzania ina matarajio makubwa ya kupata wawekezaji kutoka China hasa katika maeneo ya uwekezaji wa hoteli ili kuongeza idadi ya vitanda nchini ili kukidhi mahitaji ya watalii wanaofika nchini kutalii. Alisema kuwa utaalamu wa mafunzo kwa ajili ya rasilimali watu katika sekta ya utalii inahitajika ili kuweza kuhudumia watalii wanaofika nchi katika viwango vinavyokubalika kimataifa na hivyo kuwataka Wachina kutumia fursa hizi kuisadia Tanzania.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Bw. Allan Kijazi alisema kuwa TANAPA imeshaandaa mwongozo kwa wawekezaji unaobainisha fursa mbalimbali za uwekezaji katika Hifadhi za Taifa. Alisema kuwa mwongozo huo hivi sasa umetenga maeneo 25 kwa ajili ya uwekezaji ikiwemo manne katika Hifadhi ya Serengeti; matatu katika Hifadhi ya Tarangire; sita Hifadhi ya Katavi na manne Hifadhi ya Saadani ambako wawekezaji wanahimizwa kuwekeza ikiwemo kutoka China ambayo ukuaji wake kiuchumi unakwenda kwa kasi kubwa..

Kijazi alisema kuwa hivi sasa wawekezaji katika maeneo ya hifadhi wanatoka katika mataifa ya Marekani na Ulaya na kuwa hakuna wawekezaji kutoka China na kuwahimiza sasa kutumia fursa zilizopo katika hifadhi kwa ajili ya kuwekeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Dk. Aloyce Nzuki alihimiza mashirika ya kuratibu safari za wageni yanayomilikiwa na serikali nchini China kufungua matawi ya ofisi zao nchini ili kusaidia kuongeza idadi ya wageni kutoka China kutembelea vivutio vya utalii nchini. Alisema kuwa zipo fursa nzuri za uwekezaji ikiwemo kuanzisha safari za boti katika Ziwa Tanganyika na Victoria pamoja na safari za utalii kwa kutumia usafiri wa treni hasa katika ukanda wa Saadani na Mkomazi.

Pande zote mbili zilikubaliana kubainisha maeneo halisi ya ushirkiano na uwekezaji na kuandaa Hati ya Makubaliano ambayo itawekwa saini na pande zote ikiwa ni njia nojawapo ya kuendeleza uhusiano wa siku nyingi baina ya Tanzania na China ambao uliasisiwa na marais wa kwanza wa nchi hizi hayati  Julius Nyerere na hayati Mao Zedong.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages