MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA TUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA (COSTECH) KIJITONYAMA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA TUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA (COSTECH) KIJITONYAMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza Mkurugenzi wa Sayansi ya Uhai, Dkt. Flora Tibazarwa, wakati Makamu alipofanya ziara ya kutembelea katika maonyesho ya Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Kijitonyama leo Machi 27, 2013 kujionea maendeleo ya tume hiyo inayozalisha vijana wabunifu wa masuala ya kisayansi. Kushoto kwa Makamu wa Rais ni, Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza MMtafiti wa TEHAMA kutoka COSTECH, Rahma Bashary, wakati Makamu alipofanya ziara ya kutembelea katika maonyesho ya Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Kijitonyama leo Machi 27, 2013 kujionea maendeleo ya tume hiyo inayozalisha vijana wabunifu wa masuala ya kisayansi. Kulia ni, Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia moja ya chupa ya dawa ya kuongeza virutubisho mwilini, Juice Lishe,(Morizella Juice) huku akimsikiliza Dkt. Modest Kapingu, kuhusu matumizi ya dawa hiyo, wakati Makamu alipofanya ziara ya kutembelea katika maonyesho ya Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Kijitonyama leo Machi 27, 2013 kujionea maendeleo ya tume hiyo inayozalisha vijana wabunifu wa masuala ya kisayansi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa namna ya kutumia simu ya mkononi kuunganisha huduma ya mtumiaji simu ili kupata taarifa ya mkulima kutoka kwa Gwaliwa Mashaka wa Kampuni ya Spendid Amos, wakati Makamu alipofanya ziara ya kutembelea katika maonyesho ya Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Kijitonyama leo Machi 27, 2013 kujionea maendeleo ya tume hiyo inayozalisha vijana wabunifu wa masuala ya kisayansi. Kushoto kwa Makamu wa Rais ni, Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa maonyesho ya Kisayansi yaliyoandaliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia, leo Machi 27, 2013.Picha na OMR.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages