
Baadhi ya askari polisi wakisukuma gari lao lililoharibika katika
Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam Machi mwaka huu . Picha na
Maktaba.
---
Baadhi
ya askari polisi wa chini wanaishi maisha magumu
kutokana na kupata kipato kidogo huku wakiishi katika nyumba duni hali
inayofanya utendaji wao kushukaBaada ya shughuli nyingi za kutwa nzima,
askari polisi Hashim (siyo jina lake halisi), anarejea nyumbani
kujipumzisha.
Kwa kuwa nyumba anayoishi ipo umbali wa mita 700 kutoka katika kituo chake cha kazi, Hashim anaamua kutembea kwa miguu.
Anafika nyumbani huku akitokwa jasho mwilini,
lakini kabla ya kuingia ndani anawaza mengi, ikiwa ni pamoja na joto
lililopo katika nyumba anayoishi na mke wake pamoja na watoto wao
wawili.
Nyumba hiyo ni ya chumba kimoja na pia imeezekwa kwa mabati kuanzia juu mpaka chini.
Licha ya kukaribishwa kwa furaha na mkewe, Hashim anaingia ndani kwa unyonge, baada ya kubadili nguo za kazi anakwenda kuoga katika bafu la nje, ambalo hutumiwa na familia zaidi ya 20 za polisi wanaoishi katika nyumba za jeshi hilo (Kota) takriban 25 zilizopo Mtaa wa Mizengo (siyo jina halisi).Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea.....>>>>>>
Licha ya kukaribishwa kwa furaha na mkewe, Hashim anaingia ndani kwa unyonge, baada ya kubadili nguo za kazi anakwenda kuoga katika bafu la nje, ambalo hutumiwa na familia zaidi ya 20 za polisi wanaoishi katika nyumba za jeshi hilo (Kota) takriban 25 zilizopo Mtaa wa Mizengo (siyo jina halisi).Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea.....>>>>>>





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)