MAANDALIZI YA MWISHO YA MPAMBANO WA UZOTO MWEPESI BARANI ARIKA YAFANYIKA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAANDALIZI YA MWISHO YA MPAMBANO WA UZOTO MWEPESI BARANI ARIKA YAFANYIKA

FOR IMMEDIATE RELEASE – Friday, March 1st, 2013 -Dar-Es-Salaam,
 
 TANZANIA- Mabondia Richard Commey na Bilal Mohammed wote wa Ghana kesho watapima uzito kwenye viunga vya Lebanon katikati ya jiji la Accra, nchini Ghana kwa mpambano wao wa kutafuta Mfalwe wa uzito mwepesi katika bara la Afrika. Maandalizi haya ni pamoja na kuwaleta maofisa watakaosimamia mpambano huu ambao wote wameshawasili katika jiji la Accra wakiongozwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Masharikiu ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Baraza la Ngumi la Jumuiya ya Madola (CBC).

Maofisa wengine watakaomsaidia Ngowi ni pamona ja refarii Rodger Barnor kutoka Ghana na majaji  Fred Ghartey, Confidence Hiagbe na May Mensah Akakpo wote wanatoka katika nchi ya Ghana.
Zoezi la kupima uzito na afya za mabondia hawa litaanza rasmi saa nne asubuhi katika Hotel ya Coconut Groove Regency iliyoko karibu na Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kutoka jijini Accra.
Mpambano huu unafanyika baada ya pambano kubwa lililokuwa liwakutanishe mabondia Joseph Agbeko wa Ghana na Luis Mendelez wa Columbia nchi iliyoko Amerika ya Kusini kuhamishiwa tarehe 22 March.
Katika mpambano huu mkubwa, kulikuwa na mpambano mwingine kati ya Frederick Lawson na Isaac Sowah katika uzito wa Welter  lakini sasa utafanyika tarehe 22 March pamoja na pambano hili kubwa.
Bondia Richard Commey ni bondia anayewika kwa sasa na kupanda chati anamenejiwa na Michael Amoo-Bediako mfanyiabishara maarufu wa Ghana anayeishi katika jiji la London nchini Uingereza na kufanyiwa mazoezo na Carl Lokko wa Ghana.
Naye Bilal Mohammed bondia wa siku nyingi na mwenye madaha ulingoni anamenejiwa na kufanyiwa mazoezi na Yebohey .
ISSUED BY:
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages