Chama Cha Mapinduzi (CCM)Zanzibar:Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ifute Mara Moja Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Chama Cha Mapinduzi (CCM)Zanzibar:Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ifute Mara Moja Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI)

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mjini Magharibi, Borafya Silima.
---
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimeitaka serikali ya Mapinduzi kuifuta mara moja Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) kwa kuwa inafanya kazi kinyume na malengo yake usajili.
Kauli hiyo imetolewa jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mabata huko Magomeni Mjini Unguja na kuhudhuriwa na wanachama wa CCM na wafuasi wa CUF ambapo mgeni rasmi wa mkutano huo alikuwa ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Mjini Magharibi Borafya Silima.
Akizungumza katika mkutano huo Katibu wa Vijana wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mohammed Ali Khalifa alisema chama cha CCM kinamuomba msajili wa taasisi za kiraia achukue uamuzi wa kuifuta jumuiya hiyo ya Uamsho ili isiwepo kabisa katika kumbukumbu za asasi za kiraia hapa Zanzibar.
Alisema taasisi hiyo haiendeshi shughuli zake za kidini licha ya kuwa imesajiliwa kwa misingi ya kuendesha mambo ya dini lakini imepoteza muelekeo na imekuwa ikifanya kazi za kisiasa jambo ambalo linakwenda kinyume na malengo ya jumuiya hiyo.Aidha alisema Uamsho ina mkono wa watu wakubwa ndani ya serikali na ndio muda wote imekuwa ukinyamaziwa na hivyo kuitaka serikali kuwa macho na watendaji wake na kuwachukulia hatua wale wote ambao wamehusika katika kuwaunga mkono na kuwakamta kwa kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Kwa upande wake Mgeni rasmi wa mkutano huo, Borafya Silima alisema jeshi la polisi limefanya kazi nzuri sana ya kuhakikisha linawakamata wahalifu wote na kuwafikisha katika vyombo vya sheria na kuwataka waendelee na kazi hiyo.
Borafya alisema haiwezekani viongozi wa dini ambao hawana elimu kuachiwa kutamba na kuiharibu nchi kwa kisingizio cha kutangaza dini wakati wanachokitangaza ni siasa huku akikishutumu chama cha wananchi CUF kuwa kinahusika moja kwa moja na vurugu zilizotokea kwa kuwabariki viongozi hao wa Uamsho.
“Mtu hana dini yenyewe haijui leo hii tumwite sheikh kwani kuvaa kanzu ndio sheikh? Alihoji huku akishangiriwa na wafuasi wa chama hicho.
Mwenyekiti huyo ambaye amechaguliwa hivi karibuni amesema kwamba nafasi aliyopata ni muhimu katika siasa za Zanzibar na kwamba ataitumia vizuri na kuwataka wapinzani wake wajipange vizuri ili kukabiliana nao kwani wameingizwa madarakani kwa maridhiano.
Borafya alisema Maalim Seif amekuwa amepewa wizara zisizo na uzito wowote serikali na hivyo amekuwa akimuonea choyo makamo wa pili wa rais, Balozi Seif Ali Idd kwa kuwa yeye ndio mshughulikiaji wa wizara zote za serikali.
Mazungumzaji katika mkutano huo ambao kwa kiasi kikubwa wote waliohutubia walimlenga na kumshutumu moja kwa moja Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na kumtaka aachie ngazi kwa kuwa ameshindwa kutekeleza yale ambao aliapa kuyasimamia wakati akiingia madarakani.
Mbali na matusi ya nguoni na kumshutumu kwamba anahusika na kundi la Uamsho walisema Maalim Seif hafai kuwa kiongozi kutokana na kuwa mbinafsi kwa kuwa ameisema serikali yake mbele ya viongozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kwa kuwaeleza kwamba jeshi la polisi na vikosi vya SMZ vinahitaji mafunzo ya kukabiliana na vurugu ili waweze kupata mafunzo ya kukabiliana na vurugu hizo bila ya kuvunja haki za binaadamu.
“Huyu Maalim Seif anawaambia UNDP kwamba jeshi letu la polisi linahitaji mafunzo ya kuwakamata wahalifu sisi tunamwambia polisi wetu na vikosi vyetu havihitaji mafunzo wewe ndio unahitaji mafunzo kwa sababu kwani wewe unalindwa na nani? Si hawa hawa polisi” alisema Khalifa.
Katika hatua nyengine viongozi hao wa CCM walimtaka Maalim Seif kuachia ngazi kwa kwa kumsema rais wake Dk Shein hadharani kitendo ambacho walisema ni kwenda kinyume na kiapo chake cha kuheshimu, kulinda na kutotoa siri za serikali.
Hivi karibuni katika mkutano wake Maalim Seif alimtaka Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein kutekeleza ahadi yake ya kuwalinda wananchi wote bila ya ubaguzi na kuhakikisha vyombo vya ulinzi vinasitisha ukiukwaji wa haki za binaadamu kwa kuwa wananchi wamechoshwa na ukandamizaji wanaofanyiwa katika nchi yao.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages