Wananchi wakiitikia wito wa Maboresho ya Huduma ya LUKU nchini Tanzania - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Wananchi wakiitikia wito wa Maboresho ya Huduma ya LUKU nchini Tanzania

Waweza dhani watu hawa wapo katika foleni ya kupiga kura au kusubiri kujiandikisha kwaajili ya vitambulisho vya Utaifa..la hasha bali foleni hii ndefu ambayo huanzia majira ya alfajiri hadi usiku  wakati mwingine ni ya baadhi ya wakazi wa Ukonga jijini Dar es Salaam waliojipanga jana kupata huduma ya LUKU.

Tangu Septemba 1, 2012 Shirika la Ugavi la Umeme Tanzania (TANESCO) waliutangazia umma wa Watanania kuwa kutaanza zoezi la uboreshaji wa mfumo wa LUKU nchini. Kuanza kwa zoezi hili kumefanyika huku wananchi wakipata adha kubwa ya kukaa katika foleni kwa muda mrefu na wengine kukata tamaana kulala gizani katika nyumba zao.

Hali hii hasa ina lalamikiwa kutokana na Shirika hilo kuwa na vituo vichache vya kuuzia umeme jijini Dar es Salaam na nchi nzima kwa ujumla. Hivyo shirika halina budi kuongeza pia vituo.Picha Kwa Hisani Ya Father Kidevu Blog

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages