Spika
Makinda katikati pamoja na baadhi ya watanzania wanaoishi Italia:
kutoka kushoto ni Mhadhiri wa chuo Kikuu cha Napoli ambaye makamu
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Napoli Italia Bi Fatma
Tandika, Mwenyekiti wa jumuiya ya watazania wanaoishi Napoli, Balozi wa
Tanzania nchini Italia Dkt. James Nsekela na Afisa mwandamizi katika
Ubalozi wa Tanzania nchini Italia Bw. Msemo
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda (kulia)
akiwasili katika uwanja wa ndege wa Napoli, Italia na kulakiwa na
mwenyeji wake, Balozi wa Tanzania nchini Italia, Dkt James Nsekela leo.
Mhe. Makinda yuko nchini Italia kuhudhuria mkutao wa Shirika la Makazi
la Umoja wa Mataifa unaohusu jinsi ya kukabiliana na ukuaji wa miji
ulimwenguni. Hivyo zinahitajika juhudi za makusudi ili kuweka mipangilio
stahihiki katika miji ya Tanzania hususan majiji ya Dar es Salaam,
Mwanza na Mbeya, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu ya
usafirishaji. Ni hivi majuzi ilitangazwa kuwa Dar es Salaam ni miongoni
mwa miji inayokuwa kwa kasi kubwa barani Afrika. Ujumbe wa Tanzania
katika mkjutano huu unaongozwa na naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Goodluck Ole Medeye.Mkutano huo utaanza kesho
tarehe 2 na kuhitimishwa tarehe 6 septemba 2012.Picha na mdau Prosper Minja-Bunge






No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)