Tyson Chandler Nyota wa Kikapu Nchini USA Atua Jijini Dar es Salaam - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Tyson Chandler Nyota wa Kikapu Nchini USA Atua Jijini Dar es Salaam

Picha Juu Tyson akiwa Don Bosco wakati wa mafunzo kwa vijana wadogo/watoto wa mitaani na picha nyingine ni Mkurugenzi wa Michezo na Ushirikiano wa UNICEF USA akiwa na Magesa/TBF-VP.
---
Nyota wa Kikapu, Tyson Chandler Mchezaji mahiri wa kikapu toka Marekani anayechezea timu ya New York Knicks kama "center" na pia anachezea timu ya Taifa ya Marekani yuko jijini Dar Es Salaam kwa ziara maalumu.

Tyson yumo kwenye timu ya Taifa ya Marekani iliyotwaa medali ya dhahabu katika mashindano ya Olimpiki ya 2012 yaliyomalizika London na alicheza michezo yote.

Tyson ambaye msimu huu wa ligi ya NBA iliyoisha alichaguliwa kuwa mchazaji bora  mzuaji/Mlinzi (NBA Defensive Player of the year) pia ni balozi wa heshima wa UNICEF.

Katika ziara ya Dar amefanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kutoa mafunzo ya kikapu kwa vijana wadogo/ watoto wa mitaani katika viwanja vya Don Bosco.

Tunamshukuru sana Tyson na pia tunawashukuru UNICEF kwa ushirikiano wao.

Phares Magesa
Makamu wa Rais,
Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania(TBF).

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages