Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Said Meck Sadik muda mfupi baada ya kuwasili akitokea nchini Ghana
ambapo alishiriki mazishi ya aliyekuwa Rais wan chi hiyo Marehemu John
Atta Mills.Kushoto ni Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali
Davis Mwamnyange.
Baadhi ya watoto yatima na walemavu wakishiriki katika futari ikulu jijini Dar es Salaam jana jioni.
Rais
Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma barua aliyoandikiwa na mtoto Khaitham
Jumbe(kulia) wakati wa futari aliyowaandalia watoto walemavu na yatima
ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati anayeangalia ni mtoto Hamida Jacks
mdogo wake Khaitham. Mtoto Khaitham Jumbe ni mlemavu wa ngozi na alikuja
ikulu na wazazi wake. (Picha na Freddy Maro)
Rais
Dk. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakigawa zawadi
kwa watoto yatima na walemavu walohudhuria futari waliyowaandalia ikulu
jijini Dar es Salaam jana jioni.
Picha na Freddy Maro.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)