NMB YAFUNGUA KITUO CHA WAFANYABIASHARA JIJINI MWANZA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

NMB YAFUNGUA KITUO CHA WAFANYABIASHARA JIJINI MWANZA


Benki ya NMB imeendelea kuongeza wigo wa kutoa huduma kwa wateja kwa kuongeza matawi zaidi ya 143 na mashine za ATM zaidi ya 450 nchi nzima. Katika kuboresha huduma zake, NMB imefungua kituo maalum kwa ajili ya kuhudumia wafanyabiashara, wateja wakubwa na ofisi za serikali kiitwacho NMB Mwanza Business Center.

Kwa kupitia kituo hiki, wafanyabiashara na wateja walengwa watapata huduma kutoka mazingira yaliyo boreshwa zaidi na kwa ufanisi zaidi. NMB Mwanza Business Center ni ya tatu baada ya kituo kama hicho kufunguliwa Kariakoo, Dar es Salaam na Arusha katika jengo la Arusha Palace.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bw. Mark Wiessing alisema “Ufunguzi wa kituo hiki ni ishara kuwa NMB imejikita katika utoaji huduma bora kwa serikali, wateja wadogo, wakati na wakubwa. NMB ina mpango wa kufungua vituo vingine katika mikoa ya Mbeya na Morogoro”
 Vile vile, Benki ya NMB inatarajia kufungua tawi jipya  jijini Mwanza katika kitongoji cha Buzuruga.
 Ufunguzi huo ulifuatiwa na sherehe fupi na wateja wa NMB iliyohudhuriwa pia na Meya wa Jiji la Mwanza, Eng. Evarist Ndikilo na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Bw. Baraka Konisaga.
 Wafanyabiashara wa Mwanza Business Center wakibadilishana mawazo  wakati wa ufunguzi huo
Wafanyakazi wa NMB Mwanza Business Center wakiwa katika picha   ya  pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bw.Mark Wiessing wakati wa ufunguzi huo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages