KWA mara nyingine, Watanzania tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kuzama kwa meli ya MV. Skagit iliyotokea jirani na kisiwa cha Chumbe, Unguja. Ndugu zetu wapatao 60 tayari wameripotiwa kupoteza uhai. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa letu.
Mjengwablog, kama chombo cha jamii cha habari na mawasiliano kinatoa salamu za rambirambi
kwa wahanga wote wa msiba huu mkubwa. Na tunachukua fursa hii kumpa
mkono wa pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dr.
Jakaya Mrisho Kikwete, vivyo hivyo, mkono wetu wa pole umfikie
Mheshimiwa Dr. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Ya
Zanzibar.
Mjengwablog inaungana na Watanzania wote katika siku hizi tatu za maombelezo kwa kutorusha habari na picha za matukio yenye kuashiria sherehe na burudani.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
Maggid Mjengwa
Mtendaji Mkuu, Mjengwablog.com
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)