MJENGWABLOG INATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MJENGWABLOG INATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO


KWA mara nyingine, Watanzania  tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kuzama kwa meli ya MV. Skagit iliyotokea jirani na kisiwa cha Chumbe, Unguja. Ndugu zetu wapatao 60 tayari wameripotiwa kupoteza uhai. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa letu.

Mjengwablog, kama chombo cha jamii cha habari na mawasiliano kinatoa salamu za rambirambi kwa  wahanga wote wa msiba huu mkubwa. Na  tunachukua fursa hii kumpa mkono wa pole  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa  Dr.  Jakaya Mrisho Kikwete, vivyo hivyo, mkono wetu wa pole umfikie Mheshimiwa Dr. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Ya Zanzibar.

Mjengwablog inaungana na Watanzania wote katika siku hizi tatu za maombelezo kwa kutorusha habari na picha za matukio yenye kuashiria sherehe na burudani.
 
Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
 
Maggid Mjengwa
Mtendaji Mkuu, Mjengwablog.com

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages