Wananchi Songwa Waenda Kutibiwa na Maji Hospitalini - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wananchi Songwa Waenda Kutibiwa na Maji Hospitalini

 Mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Masagala nje kidogo ya Mji mdogo wa Maganzo, akitoka kuchota maji bwawani, bwawa hili lilichibwa na mkandarasi aliyekuwa akitengeneza barabara kwa matumizi ya ujeni.
 Lwinzi Kidiga, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Maganzo.
 Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Maganzo, Lwinzi Kidiga.
 Binti akichota maji katika moja ya mabwawa ambayo si salama kwa matumizi anuai, bwawa hili lilichibwa na mkandarasi aliyekuwa akitengeneza barabara kwa matumizi ya ujeni.
 Mabinti wakitoka kusaka maji kwa matumizi anuai.
 Binti akichota maji katika moja ya mabwawa ambayo si salama kwa matumizi anuai, bwawa hili lilichibwa na mkandarasi aliyekuwa akitengeneza barabara kwa matumizi ya ujeni.
--
 Na Joachim Mushi,

SHIDA ya maji inayoikabili Wilaya ya Kishapu imeendelea kuwabebesha wananchi mzigo pasipo kutarajia, hasa wagonjwa kwani kwa sasa wananchi wa Mji mdogo wa Maganzo Kata ya Songwa wanalazimika kwenda kutibiwa wakiwa na madumu ya maji kulingana na huduma anayoita muhusika.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi juzi mjini hapa, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Maganzo, Lwinzi Kidiga alisema wamewaelekeza wananchi kwenda kutibiwa huku wakiwa na maji kwenye madumu ili kuiwezesha Zahanati ya Maganzo kuendesha shughuli zake kwani hakuna maji katika kituo hicho.

Alisema wananchi eneo hilo hulazimika kwenda na maji kati ya madumu (ya lita 20) mawili hadi matatu kulingana na uhitaji wa maji katika huduma ambayo mgonjwa anastahili kupata jambo ambalo amekiri kuwa ni kero kwa wananchi wake.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini licha ya wananchi kulazimika kuja na maji katika zahanati hiyo pia wanapokuja kupata huduma za afya usiku hulazimika pia kuja na mafuta ya taa au tochi ambayo hutumika kuangaza wakati mgonjwa akipatiwa huduma, kwani zahanati hiyo haina umeme.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Lucas Said akizungumza na mwandishi wa habari hizi amekiri kuwepo na utaratibu wa kuwatoza maji wananchi wanaokwenda kupata huduma za afya na kudai tatizo la maji lipo kwa zahanati nyingi za eneo hilo na juhudi zinafanywa kuhakikisha huduma ya maji inapatikana maeneo anuai ya Kishapu.

Alisema kwa sasa wataalamu wanafanya utafiti katika vijiji mbalimbali kuhakikisha vinapatiwa huduma ya maji pale mpango wa kuleta maji kutoka Ziwa Victoria kwa matumizi eneo hilo utakapo kamilika. Hata hivyo ameshauri watendaji katika zahanati na vituo vya afya kuhakikisha wanajipanga vizuri katika matumizi ya fedha za ruzuku ili ziweze kugharamia huduma kama hizo na kuondoa usumbufu kwa wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Maganzo, Kidiga ilipo zahanati hiyo amesema tayari uongozi wa kijiji umefanya mazungumzo na mwekezaji wa madini ya almasi eneo hilo, mmiliki wa mgodi wa Williamson unaochimba almasi eneo hilo kuwaletea maji wananchi mradi utakaoanza kati ya mwezi Julai mwaka huu.

*Habari hii imeandaliwa na kuletwa hapa na Mtandao wa www.thehabari.com kwa kushirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP).

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages