WAKAZI WA DAR WAFURAHIA’RIDE AND DRIVE’ YA CFAO MOTORS - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

WAKAZI WA DAR WAFURAHIA’RIDE AND DRIVE’ YA CFAO MOTORS



 Moja kati ya magari ya kampuni ya CFAO Motors Group yaliyokuwa yakiendeshwa na wateja kutoka kampuni tofauti likikatiza katika mabonde wakati wa Ride & Drive yakiwemo Nissan, Benz, VW ‘AMAROK’ na Suzuki kujaribu ubora wake.
Katika msafara wa It’s Ride &ra huo piwa walikuwapo Kinamama ambao nao pia walishiriki.
 Msafara wa magari tofauti ya kampuni ya CFAO Motors Group,  yakiendeshwa na wateja kutoka kampuni tofauti wakati wa Ride & Drive yakiwemo Nissan, Benz, VW ‘AMAROK’ na Suzuki yakichanja mbuga kwenye mabonde na milima kujaribu ubora wake.
 Sales Representative wa CFAO Motors Magdalena Mpeku (wa pili kulia) na Tender Manager Bw. Marco Kahabi wakizungumza na kubadiliashana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa baada ya zoezi la Ride & Drive.
Mkurugenzi Mkuu wa CFAO Motors Uganda  Bw. Eric Ruiz akibadilishana mawazo na Meneja Masoko Mpya wa CFAO Motors Tharaia Ahmed.
********************************


Na Mwandishi wetu
Kampuni maarufu ya kuuza na kusambaza magari nchini Tanzania ya CFAO Motors kwa mara nyingine imewapa fursa wateja wake kuyajaribu kwa kuyaendesha magari wanayoyauza na gari mpya aina ya Volks Wagon katika viwanja vya maeneo ya Coco beach.

Wateja hao kutoka kampuni mbalimbali wamepata nafasi ya kupakia na pia kuyaendesha magari mapya yanayoingizwa hapa nchini na kampuni hiyo ili kujua upya na uimara wa magari hayo hivyo kuweza kuchagua magari bora ya kununua.

Akizungumza Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed amesema kampuni hiyo imechagua viwanja hivyo kwa kuwa vina sehemu zenye mawe, miinuko na barabara korofi ili wateja wao waweze kuthibitisha uimara wa magari yanayouzwa na kampuni hiyo.

Naye Mkurugenzi mpya wa kampuni mpya ya Alliance Motors Bw. Alfred Minja amesema kampuni yake ambayo ni moja ya makampuni ya CFAO Motors Group imeingiza magari mapya aina ya Volks Wagon yakiwemo ‘Amarok’ ikiwa ni katika kuwapatia watanzania nafasi ya kuchagua gari bora wanalolipenda kwa gharama nafuu.

Nao baadhi ya wateja waliopata nafasi yak u-‘Ride and Drive’ wamesifia ubora na upya wa magari hayo na kuhimiza watanzania na kampuni mbali mbli kununua gari hizo.

Dereva wa siku nyingi na mwanajeshi wa zamani Bw. Issa Swalehe amesema kuanzia gari kubwa aina ya ‘Benzi Zitros’ ni nzuri hasa katika sehemu sizizopitika kirahisi na gia zake zinaingia kirahisi kama unavyoendesha gari ndogo.

Kampuni ya CFAO Motors ambayo kwa sasa imefungua kampuni ya Alliance Motors itakayokuwa chini ya Bw. Alfred Minja na kuuza aina tofauti za magari ya ‘Volkswagon’, Nissan, Benzi na mengineyo hufanya tukio kama hilo la kutoa fursa wa wateja wake ku-‘feel’ ubora wa magari hayo mara tatu kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages