MABONDIA WAAHIDIWA BAISKELI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MABONDIA WAAHIDIWA BAISKELI

mabondia wa bigright boxing wakiwa mazoezini
kocha wa bigright boxing ibrahim akiwanoa vijana

Mabondia wa klabu ya mazoezi ya bigright ya mwananyamala wameahidiwa baiskel na katibu kata wa vijana wa CCM kinondoni REHEMA MBEGU ili ziwasaidie kwenda mashuleni mwao na mazoezini,Rehema mbegu mara nyingi huwa yupo karibu sana na vijana hao katika ushauri na kuwasaidia chakula na vinywaji wakati wakijiandaa na mashindano mbalimbali ,safari hii ameamua kutoa baiskeli ili kuhamasisha ushindani zaidi na kuwapa moyo vijana kupenda zaidi michezo kuliko vijiwe.

Baada ya kuhakikishiwa kuwa kila bondia atakae shinda toka klabu ya ngumi ya bigright atazawadiwa baskeli,wameahidi kukatika mikono ulingoni yaani ni lazima washinde na wamebadilisha mfumo mzima wa mazoezi,kwa sasa wapo pamoja,kikambi zaidi nyumbani kwa kocha wao Ibrahim bigright na kuongeza muda zaidi wa mazoezi kwa sasa wanafanya mara tatu hadi nne kwa siku.

Mabondia hao ambao wanategemea kupanda ulingoni july 15 DDC-kariakoo ni Issa Omar(bigright boxing) atakaechapana na Ramadhan Kumbele toka kambi ya matumla katika uzani wa fly,Mwaite juma toka bigright boxing atapigana na mkongwe Anthony Mathias katika uzani wa bantam.

Ambao watakuwa wakisindikiza pambano la ubingwa wa taifa kati ya JUMA FUNDI wa keko na BAINA MAZOLA wa mabibo toka kambi ya mzazi
 
mapambano hayo yameandaliwa na kaike siraju na kusimamiwa na TPBO

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages