Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akizungumza jambo na mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwasa wakati wa sherehe
za ufungaji wa awamu ya kwanza ya utengaji wa maeneo ya sensa ya watu na makazi
katika viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora.
Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza
kupatikana mara moja akiwa katika viwanja vya Chipukizi mjini Tabora kushuhudia
ufungaji wa awamu ya kwanza ya utengaji wa maeneo ya Sensa ya watu na Makazi.
Vijana wa kikosi cha ulinzi wa jadi cha Sungusungu
(waliokaa chini) pamoja na wananchi wa mkoa wa Tabora wakifuatilia zoezi la
ufungaji wa awamu ya kwanza ya utengaji wa maeneo ya sensa ya watu na makazi
mkoani Tabora.
Wadau wa sensa ya watu na makazi 2012 Bw. Bakari
Kimwanga kutoka gazeti la Mtanzania (kushoto) na Bw. Said Ameir kutoka Ofisi ya
taifa ya Takwimu (kulia) wakiwa ndani ya msitu wa tula wilayani Uyui kwenye barabara kuu itokayo mkoani Tabora
mara baada ya kukamilika kwa shughuli za ufungaji wa awamu ya kwanza ya
utengaji wa maeneo ya sensa ya watu na
makazi zilizofanyika kitaifa mkoani humo.(PICHA NA ARON MSIGWA WA MAELEZO)
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)