Maggid Mjengwa Neno La Leo: Siku Hiyo Inakuja... - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Maggid Mjengwa Neno La Leo: Siku Hiyo Inakuja...

 Usafri wa treni utakuwa wa uhakika zaidi kuliko ilivyo sasa. Kwamba wengi tutachagua kusafiri kwa treni kwa vile ni nafuu zaidi na salama zaidi. Na ni usafiri rafiki kwa mazingira. 

Siku hiyo inakuja kwa vile tunachoshindwa sasa ni kuwepo kwa wachache ' wanaohujumu' kwa makusudi usafiri wetu wa njia ya reli. 

Mapato yanayopatikana yanapotea. Kuna abiria wanaosafiri bila nauli zao kuingia kwenye Shirika bali kwenye mifuko ya wanaojiita wajanja. Kuna mizigo pia inayosafirishwa bila mapato yake kuingia kwenye Shirika, bali, kwenye mifuko ya wanaojiita wajanja. Hali hiyo ni kwa reli ya kati na reli ya Uhuru pia, kwa maana ya Tazara.

Na hao wanaojiita wajanja wengine ni viongozi tuliowapa dhamana za kusimamia mashirika yetu ya umma.

Siku hiyo inakuja tutakapokuwa na mfumo utakaohakikisha mwisho wa wanaojiita wajanja.

Hivyo basi, siku hiyo inakuja tutakapoona fahari kusafiri kwa njia ya reli yanayooendeshwa na mashirika yetu ya umma chini ya uongozi wa wazalendo wa nchi hii watakaokuwa tayari hata kutoa fedha za mifukoni mwao kuhakikisha treni zinatembea kwenye reli zetu.

Naam, siku hiyo inakuja....
Na hili ni Neno La Leo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages