*MASHABIKI WA KLABU YA SIMBA KUJISHINDIA BAJAJI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

*MASHABIKI WA KLABU YA SIMBA KUJISHINDIA BAJAJI

Meneja kampeni wa kampuni ya Push Mobile, Talib Rashid (katikati) akifafanua jambo kuhusiana na Bahati Nasbu ya Simba kwa kutumia ujumbe mfupi wa meseji ambapo mshindi atazawadiwa pikipiki aina ya Bajaj. Zawadi nyingine katika bahati nasibu hiyo ni pikipiki na fedha taslim Sh. 50,000 zitakazotolewa kila siku kwa muda wa siku 90. Kulia ni Katibu Mkuu wa Simba Evodius Mtawala na kushoto ni Swed Mkwabi ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendai ya klabu hiyo. Picha na Mpiga picha wetu
***************************************

Na Mwandishi wetu
KAMPUNI ya Push Mobile kwa kushirikiana na klabu ya Simba imezindua kampeni ya bahati nasibu kwa mashabiki wa timu hiyo ambapo mshindi atajinyakulia pikipiki aina ya bajaji yenye thamani ya Tsh 6 Milioni.
Akizindua kampeni hiyo leo kwenye ofisi za Push Mobile Kinondoni jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala alisema kampeni hiyo itasaidia kuwaweka pamoja na wanachama wa klabu hiyo kongwe hapa nchini.
Mtawala alisema falsafa ya simba ambayo ni timu ya wananchi ni kuwa karibu na wanachama wake popote duniani hivyo kampeni hiyo itasaidia kuiweka karibu zaidi klabu hiyo na wanachama wake .
Naye Meneja wa Kampeni hiyo kutoka Push Mobile, Talib Rashid alisema droo kubwa ya bahati nasibu hiyo itachezeshwa baada ya siku 90 na mashabiki wa simba wanatakiwa kuandika ujumbe mfupi wa maneno (SMS) yenye neno Simba na kuituma kwenda namba 15678 ili kuingia katika droo hiyo.
Rashid alisema mbali na zawadi hiyo pia mashabiki hao watajinyakulia zawadi ya pesa taslimu tsh 50,000 kila siku ndani ya siku 90 pia washindi wengine wawili watajinyakulia pikipiki zenye thamani ya tsh 1.5 Milioni kila moja.
"Kampeni hii itahusisha mashabiki wa klabu ya simba ambao watatakiwa kujibu maswali ambayo baada ya kutuma neno Simba kwenda namba 15678 watatumia kwenye simu zao," alisema Rashid.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages