Iddi Seif Sandaly Rais Mpya Wa Chama Cha Watanzania DMV - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

Iddi Seif Sandaly Rais Mpya Wa Chama Cha Watanzania DMV

IMG_9725
Iddi Seif Sandaly ndiye rais mpya aliyechaguliwa kwenye mkutano wa uchaguzi wa Watanzania DMV uliofanyika katika ukumbi wa Mirage, Iddi Seif Sandaly alishinda kwa kura 205.
IMG_9724
Jacop Kinyemi aliyekuwa kwenye kinyang'anyiro cha Ukatibu Mkuu na kuwa wa pili kwa kura 82, Amos Cherehani ndiye aliyeshinda Ukatibu Mkuu kwa kura 192 na Rhoda Kasamba kwenye nafasi ya Ukatibu Mkuu alipata kura 40.
IMG_9721
Loveness Edwin Mamuya ambaye alikuwa mgombea wa Urais kwenye mkutano wa uchaguzi uliofanyika Jumapili Aprili 15, 2012 na kupata kura 119.
IMG_9623
 Mselem (kushoto) na Dr. Mwamoyo Hamza, Kamati ya Kurekebisha Katiba ambayo pia ilisimamia uchaguzi wakitayarisha vitendea kazi na kuweka mambo sawa kabla ya upigaji kura.
IMG_9619
 Mgombea Uraisi Loveness Mamuya (kati) akifuatilia mkutano wa uchaguzi
IMG_9618
Maafisa Ubalozi wakifuatilia uchaguzi huo.
IMG_9635
 Watanzania wa DMV wakiwa mkutanoni.
IMG_9636
 Watanzania wa DMV ambao Jumapili Aprili 15, 2012 walifika kwa wingi na kuandika historia mpya kwa kuwachagua viongozi watakaoongoza Jumuiya DMV ambayo ilikuwa inalegalega tangia 2007.
IMG_9624
 Mgombea wa Urais Iddi Sandaly (kati) akifuatilia mkutano wa uchaguzi.
IMG_9667
Wajumbe wa Bodi ambao wote walipita kwenye uchaguzi huo kutoka kushoto ni Al- Amini Chande, Dr. Hamza Mwamoyo, Eliserena Kimolo, Grace Sebo Mgaza na Haruni Ulotu.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages