BENKI YA NBC YATOA MSAADA WA VIFAA VYA TIBA NA KUJITOLEA KUFANYA USAFI MAENEO YA HOSPITALI YA TEMEKE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

BENKI YA NBC YATOA MSAADA WA VIFAA VYA TIBA NA KUJITOLEA KUFANYA USAFI MAENEO YA HOSPITALI YA TEMEKE

01M
 Mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Temeke, Zainabu Abbasi pamoja na mwanawe, Kheri Hasifu wakipokea boksi la sabuni ya kufulia kutoka kwa Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Ilala, Gaudence Shawa, wakati wafanyakazi wa NBC walipofika hospitalini hapo kukabidhi msaada wa vifaa vya tiba na sabuni na kushiriki shughuli za usafi jan. Kulia ni Katibu wa Afya wa hospitali hiyo, Lucy Sozigwa.
03N
 Mmoja wa wafanyakazi wa benki ya NBC, Ali Lwano,  akigawa sabuni kwa baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Temeke, wakati wa hafla hiyo fupi ambayo NBC ilikabidhi msaada wa vifaa vya tiba na sabuni na kushiriki shughuli za usafi hospitalini hapo.
04M
 Wafanyakazi wa benki ya NBC, Janeth Mutahanamilwa (katikati) na Emmanuel Mseti (kulia kwake) wakigawa sabuni kwa baadhi ya wagonjwa na watoto wao waliolazwa katika Hospitali ya Temeke.
05M
  Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya NBC wa Kanda ya Ilala wakisafisha mazingira ya hospitali hiyo wakati wa hafla hiyo.
06,M
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya NBC wa Kanda ya Ilala na watumishi wa Hospitali ya Temeke wakipozi kwa picha katika hafla ambayo NBC ilikabidhi msaada wa vifaa vya tiba na sabuni na  kushiriki shughuli za usafi hospitalini hapo Dar es Salaam jana. Matawi yaliyoshiriki katika hafla hiyo ni,  hiyo Corporate, Mnazi Mmoja, Kichwele, Samora, Industrial, Kariakoo, Muhimbili, Chang’ombe na Mbagala.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages