KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL),
imesitisha udhamini wake kwa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars
ulioanza mwaka 2006 kufuatia kupandishiwa dau la kuidhamini timu hiyo na
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Habari za kiuchunguzi, ambazo
zimepatikana zimesema kwamba SBL iliyoanza kuidhamini Taifa Stars kwa
dau la Sh. Milioni 700, imetakiwa na TFF kutoa Sh. Bilioni 3.6 kwa mwaka
kuidhamini timu hiyo.
Ofisa mmoja wa TFF, ambaye hakutaka
kutajwa jina alisema jana kwamba pamoja na hayo mazungumzo
bado yanaendelea baina ya SBL na shirikisho hilo'
Hata hivyo, Ofisa huyo wa TFF alisema shirikisho limeahidiwa udhamini mnono kutoka kampuni nyingine kubwa ya bia nchini.
"Lakini kwa kuzingatia pale ambapo SBL
wameitoa Taifa Stars, waliichukua haina mdhamini na hakuna mtu au
kampuni iliyokuwa tayari kuidhamini, wamefanya mambo mengi kwa manufaa
ya soka hii, kwa kweli hata mimi ningependa SBL iendelee kudhamini timu
hii,"alisema Ofisa huyo.
TFF iliipandishia dau la udhamini SBL kutoka Milioni 700 hadi 800, baadaye 900 na mwaka jana ilikuwa ni Sh Bilioni 1.2.
TFF sasa inataka Sh Bilioni 3.6 kwa
mwaka na kwa sababu mkataba wa udhamin baina ya pande hizo mbili uliisha
tangu Desemba, Taifa Stars haina mdhamini kwa sasa.
Teddy Mapunda, Mkurugenzi wa
Mawasiliano na Mahusiano wa SBL alipoulizwa kuhusu mustakabali wa suala
hilo, alikiri kwa sasa mambo yote yamesimama kwa sababu mazungumzo
yanaendelea kati yao na TFF.






No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)