MWILI WA KATIBU MKUU MSAIDIZI WA TUSA KUWASILI TAREHE 20/03/12 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MWILI WA KATIBU MKUU MSAIDIZI WA TUSA KUWASILI TAREHE 20/03/12

Aliyekuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa TUSA, Andrea Lesso Hange, enzi za uhai wake.
Ndugu Wanachama, wana michezo na Watanzania kwa Ujumla.
TAARIFA YA MSIBA WA ALIYEKUWA KATIBU MKUU MSAIDIZI MAREHEMU ANDREA HANGE (1970-2012)

Kwa niaba ya Shirikisho la michezo la vyuo Vikuu Tanzania(Tanzania University Sports Association)

Nawataarifu kuwa tulipokea kwa masikitiko makubwa msiba wa Kiongozi mwenzetu wa TUSA, Mpendwa wetu Ndg. Andrea Lesso Hange ambaye hadi kifo chake alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa TUSA na Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kifo chake  Kilitokea tarehe 02/03/2012 huko Swedeni alikokuwa masomoni. Taarifa tulizonazo ni kuwa mwili wake ulikutwa chumbani kwake. Uchunguzi wa kifo chake bado unaendelea.

Taarifa tulizo nazo kama chama ni kuwa mwili utawasili hapa nchini tarehe 20/03/12 na unatarajiwa kuzikwa tarehe 21/03/12 Kwa hivi sasa Msiba upo nyumbani kwake Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Karibu na Hall One.

Tunawaomba wanachama wote wa TUSA, wanafunzi wote waliosoma Elimu kwa michezo nyakati tofauti pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wanamichezo wote na watanzania kwa ujumla tukutane wote kwa pamoja tarehe 19/03/12 ili kufanikisha shughuli hii.

Watu wote tushirikiane katika kipindi hiki kigumu kwani mwili umesubiriwa kwa muda mrefu na gharama zimekuwa kubwa.

Pia unaombwa kutembelea Blog ya TUSA (http://tusadailyblog.blogspot.com/) kwa kupata taarifa nyinginezo kuhusu msiba huu.

Asante Sana kwa Ushiriakiano Wenu
NOEL KIUNSI
KATIBU MKUU TUSA

NOEL B. KIUNSI
PRINCIPAL GAMES TUTOR
UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
P.O. BOX 35091
DAR ES SALAAM
TANZANIA

+255713263556

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages