Mkuu Mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba aapishwa Ikulu leo - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Mkuu Mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba aapishwa Ikulu leo

 Mkuu Mpya wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) Meja Jenerali Samwel Ndomba akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikweteikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Meja Jenerali Ndomba anachukua nafasi yaMeja Jenerali Samwel Kitundu aliyestaafu hivi karibuni kwa mujibu wa sheria.
 Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi mkuu mpya wa JKT meja Jenerali Samwel Ndombawakati wa hafla ya kumuapisha iliyofanyika leo asubuhi ikulu jijini Dar esSalaam.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,(kushoto)Waziri Mkuu Mizengo Pinda(kulia) na Mkuu mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba wakiwakatika picha ya pamoja muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha mkuu huyo mpyawa JKT ikulu jijini Dar es Salaam leo.
 Amiri Jeshi mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(Katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange(kushoto) na Mkuu mpya wa JKT Meja Jenerali Samwel Ndomba muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mzeeAlbert Ndomba(85),baba mzazi wa Mkuu Mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba(wapili kushoto) baada ya halfa ya kumuapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni mke wa Meja Jenerali Ndomba na waliosimama nyuma ni wanafamilia.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages