Precision Air yafanya mabadiliko katika safari zake Johannesburg - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Precision Air yafanya mabadiliko katika safari zake Johannesburg



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Precision Air yafanya mabadiliko katika safari zake Johannesburg

Dar es Salaam, Februari 24 2012. Precision Air- Shirika la ndege linaloongoza Tanzania leo imetangaza kufanya mabadiliko katika ratiba yake ya safari kwenda Johannesburg, ambapo itaanza kuondoka saa 11 jioni badala ya saa 2 kama hapo awali kwa ajili yakuwezesha wasafiri wake kuweza kuwahi na kuwapatia urahisi wa kuunganisha safari kwenda kwingine.

Akizungumza katika makao makuu ya shirika hilo Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Biashara Bw. Patrick Ndekana amesema kwamba uamuzi huo umekuja baada ya utafiti uliofanywa na shirika hilo, ambayo imependekeza kwamba watumizi wa huduma hiyo wanapendelea kusafiri mapema kwa ajili ya kupata urahisi wa kuunganisha safari kwenda kwingine, pamoja na kujihakikishia usalama kwa wanaoishia uwanja wa kimataifa Oliver Tambo jijini Johannesburg.  
 
 “Kaunzia Februari tarehe 29 mwaka huu tutaanza kuondoka Dar es Salaam saa 11 jioni na kufika jijini Johannesburg saa 1:45 usiku,” alisema Bw. Ndekana.
“Tunaamini kwamba mabadiliko haya ya ratiba yatavutia idadi kubwa ya wasafiri pamoja na kutuongezea biashara nzuri zaidi kwa shirika letu,” aliongeza.

Mkurugenzi huyo pia alisema kwamba pamoja na kufanyika kwa mabadiliko hayo, muda wa kurejea kutoka Johannesburg kuja Dar es Salaam hautabadilishwa. “Muda wa kutokea Johannesburg utabakia pale pale saa 5:50 na kufika Dar es Salaam saa 10:20 alfajiri,” alisema.

Kwa mujibu wa Bw. Ndekana mabadiliko hayo yanaashiria pia kwamba Precision Air wana umakini wa kusikiliza na kuchukulia maanani mawazo mbali mbali kutoka kwa wateja wake.  

“Kama shirika la umma iliyoorodheshwa katika soko la hisa la Dar es Salaam kupokea maoni mbali mbali kutoka kwa wanahisa na wadau wetu ni jambo jema, ambayo tunaamini kwamba inatuongezea thamani kubwa kama shirika la ndege,” alisema.
Wakati huo huo, shirika hili ikishirikiana na shirika la ndege la Kenya Airways imeweza kuongeza idadi ya safari za moja kwa moja baina ya Dar es Salaam na Nairobi kutokea 4 hadi 5 kwa siku. 

Akizungumzia nyongeza hiyo Bw. Ndekana amesema kwamba safari hizo zitafanyika kwa kushirikiana na Kenya Airways, ambao shirika hilo la Kenya litaratibu safari 2 wakitumia ndege aina ya Embraer 190 (E190) wakati Precision Air wakiratibu safari 3 kutumia ndege yao ya B733.

“Jambo la kuvutia katika hizi safari ni kwamba zote zitatumia ndege aina ya Jet, na sio ATR’s, ambayo inamaanisha usafiri murua zaidi kwa wateja wetu maana watatumia muda mfupi wakiwa angani,” alisema.

Safari ya nyongeza ya Nairobi kutokea Dar es Salaam inatarajiwa kuanza sawia na mabadilko ya safari ya Johannesburg, tarehe 29 Februari, 2012.
“Kuna idadi kubwa ya wasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Nairobi, na  kurudi – ambayo inajumuisha wafanyabiashara na wafanyakazi wa makampuni kutoka sekta mbali mbali,” aliongeza Ndekana. 

Shirika la ndege la Precision Air ina mtandao mkubwa nchini kuliko mashirika yote Tanzania, ikiwa inafanya safari kwenda;  Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Zanzibar, Mwanza, Bukoba, Kigoma, Tabora, Musoma, Shinyanga, Mtwara. Kikanda Precision Air inasafiri kwenda   Nairobi, Mombasa, Entebbe, Hahaya na Johannesburg.

                        Mwisho.                             

                              Imetolewa na Ofisi ya Mawasiliano.                              Tel: 0786 404 010/0712 223 839

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages