Msanii wa Hip Hip anayewakilisha kundi la Chemba Squad, Albert Mangwair. akikamua stejini. WASANII wa muziki wa Bongo Fleva jana walishusha bonge la shoo katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, katika kuukaribisha mwaka mpya 2012. Hafla hiyo iliyofahamika kama ‘Bongo 50’ iliandaliwa na kituo cha radio cha Clouds FM kikishirikiana na mtandao wa simu za mkononi wa Airtel.
Mwana-Hip Hop toka jiji la Mwanza, Fareed Kubanda ‘Fid Q’ akiwa nyuma ya steji.
Msanii Dogo Aslay ambaye ni zao la Mkubwa Fela kutoka ‘crew’ ya Wanaume, akifanya vitu vyake.
P Funk akiwasambazia washikaji wake shampeni.
DJ Ziro akihakikisha sauti za muziki ziko 'swaafi'.
Matataki yakirushwa mtindo mmoja ilipofika saa sita kamili.
PICHA ZOTE NA ERICK EVARIST/GPL





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)