TAASISI MBALIMBALI ZACHANGIA MFUKO WA HASSAN MAAJAR TRUST USIKU HUU - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

TAASISI MBALIMBALI ZACHANGIA MFUKO WA HASSAN MAAJAR TRUST USIKU HUU

Balozi Mwanaidi Maajar ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi Hassan Maajar Trust akizungumza katika hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua madawati katika shule mbalimbali nchini iliyoandaliwa na taasisi hiyo, hafla hiyo inafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu, na imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wastaafu wa serikali pamoja na baadhi ya mawaziri na wakuu wa makampuni mbalimbali jijini Dar es salaam. Kauli mbiu ya hafla hiyo ni A Desk For Every Child.
Waziri Mkuu mstaafu Fredirick Sumaye akisalimiana na Balozi Mawaidi Maajar wakati Mh. Sumaye alipowasili ukumbini hapo, kulia ni Mama Esther Sumaye.
Waziri Mkuu mstaafu Joseph Sinde Warioba kulia akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Kampuni ya bia ya Serenget SBL Mzee Mark Bomani. Balozi Mwanaidi Maajar akisalimiana na wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyo usiku huu. 
Hawa ndiyo viongozi wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust wakiwa katika picha ya pamoja wakati walipokuwa wakitambulishwa na Balozi Mwanaidi Maajar.Picha Kwa Hisani Ya Full Shangwe Blogu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages