Mkurugenzi Mkuu-Dkt Albina Chuwa
TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA UMMA
CHAPISHO LA PATO LA MKOA WA IRINGA
Utayarishaji wa Pato la Mkoa wa
Iringa umekamilika
Kazi hii imefanywa na Ofisi ya Taifa
ya Takwimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa.
Kazi kubwa ilikuwa ni ukusanyaji wa
taarifa ya uzalishaji wa bidhaa na huduma katika Mkoa wa Iringa kwa miaka
iliyokusudiwa ambayo ni mwaka 2006, 2007
na 2008.
Dhumuni kuu ni kutoa viashiria vya
Pato la Mkoa, Pato la Wilaya ya Wastani wa Pato kwa Mkazi ambayo vitatumika
katika kutathmini sera mbalimbali ikiwa ni pamoja na hali ya umaskini katika
Mkoa wa Iringa.
Matokeo haya yatatangazwa rasmi 20
Desemba, 2011 katika mkutano wa wataalamu wa Mkoa wa Iringa (RCC) tarehe 20
Desemba, 2011 mnakaribishwa.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu inahimiza
wote kuwa kutoa Pato la Mkoa wa Iringa itakuwa ni chachu kwa Mikoa mingine
ambayo haijafanya zoezi hili.
TAKWIMU KWA MAENDELEO
ASANTENI
Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Taifa ya
Takwimu
S. L. P. 796 Dar es Salaam.
Simu +255 22 2122724, +255 22
2122722/3
Fax:
+255 22 2130852
Barua pepe: dg@nbs.go.tz
Tovuti: www.nbs.go.tz






No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)