MAKAMUZI ZAIDI KATIKA UZINDUZI WA AIRTEL MONEY JIJINI MBEYA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAKAMUZI ZAIDI KATIKA UZINDUZI WA AIRTEL MONEY JIJINI MBEYA

Mkali wa muziki wa hip hop kwenye anga ya muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Mflame wa Rhymes, Simba Mzee, Afande Sele akiwarusha vilivyo wakazi mbalimbali wa jiji la Mbeya, waliojitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel, Airtel Money uliofanyika jana jioni kwenye uwanja wa mpira wa miguu wa Sokoine.
Kundi la muziki wa kizazi kipya kutoka Temeke, Wanaume Halisi likiongozwa na kinara wao Juma Nature wakilishambulia jukwaa vilivyo jan jioni ndani ya uwanja wa Sokoine, kwenye uzinduzi wa huduma mpya itolewayo na kampuni ya simu ya mikononi ya Airtel, ijulikanayo kwa jina la Airtel Money, ambapo wakazi wa jiji la Mbeya wameipokea kwa shangwe.
Ilikuwa shangwe mwanzo mwisho, wakazi wa Mbeya wameipokea vyema huduma ya Airtel Money.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Jaffarai akitumbuiza jukwaani jana jioni kwenye tamasha la uzinduzi wa huduma mpya kutoka kampuni ya simu ya Airtel, ijulikanayo kwa jina la Airtel Money.
Wakazi wa jiji la Mbeya kutoka vitongoji mbalimbali wakishangilia vilivyo jana jioni kwenye tamasha hilo la Airtel Money, lililofanyika katika uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Jukwaani ni wakali wa miondoko ya hip hop katika muziki wa kizazi kipya, kulia ni Jaffarai pamoja na Jay Mo wakikamua vilivyo jukwaani kwenye tamasha la Bongo 50, lililodhaminiwa na kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel, kupitia huduma yao mpya ya Airtel Money.
Palikuwa hapatoshi kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya. Picha Zote na Ahmad Issa Michuzi MICHUZI JUNIOR

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages