Halima Mchuka (katikati) akizungumza jambo enzi za uhai wake . Kulia ni Eda Sanga aliyekuwa bosi wake .
MTANGAZAJI
wa muda mrefu wa iliyokuwa Redio Tanzania Dar esSalaam RTD na baadae
Shirika la Utangazaji Tanzania (SHIUTA) amefariki Dunia. Taarifa
zilizopatikana hivi punde zinadai kuwa Mtangazaji huyo ambaye
alikuwa na kipaji kikubwa cha utangazaji amefariki Usiku huu wa
leo tarehe 29-12-2011 saa 9.00alfajiri kutokana na kupatwa na
stroke ya gafla .
“Alikuwa
na tatizo hilo jana mchana mara baada ya kutangaza kipindi cha
salaam cha TBC-Taifa na akazidiwa ndipo alipopelekwa Hospitali na
sasa ndiyo amefariki dunia.”alibainisha mmoja wa watangazaji wa TBC
ambaye alikuwa jirani na mtangazji huyu. Halima Mchuka
inaaminika kuwa alijiunga na Radio Tanzania Dar es Salaam mwaka
1994 ambapo alifanya kazi katika idara ya Habari na idara ya
mipango.
Wadau
wengi wa RTD na baadae TBC-Taifa wanamkumbuka sana mama huyu wa watoto
wawili kwa kuwa mwanamke wa awali kuangaza mpira katika ukanda
wetu huu wa Afrika Mashariki na kati.
“Unapotaja
mpira wa miguu wakai huu huwezi kusahau kipindi cha michezo cha RTD cha
saa mbili kasorobo na huyu dada Halima Mchuka.”alibainisha Idd Pazi
mmojawapo wachezaji nguli wa Tanzania wa wakati huo.
Kwa
hakika si wasikilizaji wa RTD na wanamichezo tu bali ata watu wa
Karibu ambao waliwahi kufanya nae kazi tunamtazama kuwa ni
mtu mpole mwenye huruma na kusaidia wenzake pale penye tatizo
ambalo yeye anaweza kulitatua.
”unajua
huyu mama mimi ndiye aliyenisaidia kuweza kupata kazi kwenye
taasisi hii nilikuwa wala simfahamu mtu ,amenisaidia sana.”kuficha
ni dhambi alinidokeza mfanyakazi mmoja wa SHIUTA.
Mara
ya mwisho kuongea na mwana mama huyu nilikuwa nikiwa Iringa
alinipigia simu na kuniulizia taarifa za familia yangu na kuniambia
nimtunze sana mtoto wangu lakini huku akiniambia na kutambua “
mbona leo unaongea kwa unyonge” ah “ Halima hapana ila nipo eneo
ambalo watu wanasoma ndiyo maana naongea kwa sauti ya chini
“nilimjibu wakati huo kwani nilikuwa makaba ya Chuo Kikuu cha
Tumaini Makumira- Iringa.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)