Friday, December 23, 2011 BASATA: WASANII FANYENI UTAFITI KUBORESHA KAZI ZENU - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, December 23, 2011 BASATA: WASANII FANYENI UTAFITI KUBORESHA KAZI ZENU

Mdau wa Jukwaa la Sanaa ambaye pia ni Mjumbe wa Shirikisho la Muziki, Francis Kaswahili akifafanua masuala mbalimbali kuhusu Utafiti kwenye Sekta ya Sanaa.
Na  Aristide Kwizela
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeeleza kuwa, kuna kila sababu ya Wasanii kufanya utafiti wa kina kabla ya kuandaa kazi zao ili zikubalike kwa walaji na si kujifurahisha wao wenyewe.
  Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Habari wa BASATA, Godfrey Lebejo (Katikati) akizungumza na Wadau wa Jukwaa la Sanaa wiki hii kuhusu umuhimu wa Utafiti kwenye sekta ya Sanaa. Kulia ni Mratibu wa Jukwaa la Sanaa, Aristide Kwizela na Kaluona Desdery

Wito huo umetolewa wiki hii na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari BASATA, Godfrey Lebejo wakati akizungumza na Wadau wa Sanaa katika ukumbi wa BASATA uliopo Ilala Bungoni kwenye program ya Jukwaa la Sanaa.

Lebejo alisema kuwa, utafiti ni muhimu pale msanii anapotafuta wazo la kuandaa kazi ili kujua itakubalika kiasi gani kwa jamii na ni ujumbe wa namna gani unakusudiwa.

“Msanii lazima afanye utafiti ili ajue mlaji wa kazi yake anataka nini. Hauwezi kutengeneza kazi ili kujifurahisha mwenyewe mwisho wa siku mlaji ni jamii inayokuzunguka” alisema Lebejo.

Aliongeza kuwa, madhara ya wasanii kutofanya utafiti husababisha kazi zao zisikubalike kwa jamii, zikose masoko, zidumu kwa muda mfupi lakini pia kuipotosha jamii kwa ujumla wake.

Aidha, aliongeza kuwa, vilio vya wasanii juu ya ukosefu wa masoko ya kazi zao, kujirudiarudia kwa kazi hizo na matatizo ya kunakili havitakwisha ikiwa wasanii hawatokuwa tayari kutumia muda wao katika kufanya utafiti. Alisisitiza kuwa, utafiti ni moja ya mbinu za kutafuta maarifa mapya na suluhisho juu ya matatizo au changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii hususani wasanii na sekta ya Sanaa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages