Baadhi
ya wafanyakazi na wanafamilia wa benki ya NBC wakishindana katika
mchezo wa kufukuza kuku katika Siku ya Wanafamilia ya benki hiyo katika
Hoteli ya South Beach, Dar es Salaam. Mshindi wa mbio hizo huondoka na
kuku huyo na kwenda nae kumfanya kitoweo au kumfuga.
Baadhi ya watoto wa wafanyakazi wa benki ya NBC wakifurahi katika bwawa
la kuogelea ikiwa ni baadhi ya burudani kuadhimisha Siku ya Wanafamilia
ya benki hiyo katika Hoteli ya South Beach, Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya NBC, Lawrence Mafuru (kushoto) akishiriki kusakata
dansi lililokuwa likiporomoshwa na bendi ya FM Academia ‘Wazee wa
Ngwasuma’ wakati wa sherehe za Siku ya Wanafamilia wa benki hiyo katika
Hoteli ya South Beach, Dar es Salaam.
Ofisa Uhusiano wa NBC, Eddie Mhina akigawa zawadi kwa baadhi ya watoto
wa wafanyakazi wa benki hiyo wakati wa sherehe za Siku ya Wanafamilia
wa benki hiyo jijini Dar es Salaam.

No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)