AJALI TATU ZATOKEA BARABARA YA MANDELA DAR, MOJA YAUA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

AJALI TATU ZATOKEA BARABARA YA MANDELA DAR, MOJA YAUA

Teksi yenye namba T602 AFR ikiwa imeharibika vibaya.
Watu waliofika eneo la ajali hiyo.
MTU mmoja amefariki katika moja ya ajali tatu zilizotokea leo katika Barabara ya Mandela, jijini Dar es Salaam ambapo  mwendesha pikipiki alishindwa kuimiliki mashine yake hiyo na kuliingia gari kwa aina ya Toyota Coasta kwa nyuma na kufa papo hapo.

Ajali nyingine  ni magari ya jeshi la wananchi yamegongana baada ya gari la mbele kushika breki ghafla. Hata hivyo, hakuna mtu aliyejeruhiwa.


Ajali ya tatu  ilikuwa kati ya daladala  aina ya Toyota DCM lifanyalo safari zake kati ya Ubungo na Gongo la Mboto liligongana na teksi na kusababisha teksi hiyo kuharibika vibaya lakini hakuna aliyejeruhiwa.
 
Teksi inavyoonekana kwa mbele.
 
Askari wa usalama aliyefika eneo la ajali.
 
Muonekano wa gari kwa nyuma.
 
Daladala la DCM ambalo halikuharibika sana.
 
Wananchi wakiangalia gari lililo pata ajali.
HABARI/PICHA NA HARUN SANCHAWA, GPL

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages